Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SIMBA YALIA NA YANGA, AZAM NA TFF

Na Saida Salum

Klabu ya Simba imeendelea kulalamikia ratiba ya ligi kuu bara inavyopanguliwa kila kukicha ikiwa na malengo ya kuzibeba Yanga na Azam.

Hajji Manara msemaji wa klabu hiyo ameishutumu TFF kwa kuonyesha waziwazi kuzibeba Yanga na Azam kwa kuziondolea mechi zake za ligi kuu bara hivyo sasa utakuwa mtihani mkubwa kwao.

Simba ibaongoza ligi hiyo kwa kukusanya pointi 54 lakini imeshuka dimbani mara 22 ikiwa ni tofauti ya mechi mbili na Yanga na mechi tatu na Azam.

Yanga ina pointi 50 wakati Azam ina pointi 47, kwahiyo kama itacheza na kushinda mechi zake tatu zilizosalia itafikisha pointi 56 na itakuwa imeishusha Simba katika nafasi yake ya kwanza.

Yanga nao wakishinda mechi zao mbili watafikisha pointi 56 na wataishusha Simba katika nafasi yake ya kwanza, Manara ameshangazwa na kitendo cha TFF kuzifutia Yanga na Azam mechi zake za ligi zilizopangwa kuchezwa hivi karibuni.

Msemaji huyo amedai hakuna ligi yoyote duniani inayosogezwa mbele kwa sababu kuna timu inashiriki michuano ya kimataifa, ameongeza kuwa hiyo ipo hapa Tanzania pekee na si kwingineko.

Hata hivyo Manara amedai hiyo ni mbeleko ya kuzibeba Yanga na Azam, Yanga haitacheza tena ligi mwezi huu na itasubiri hadi mwezi ujao, wakati Azam itacheza mchezo mmoja tu kisha itasubiri hadi mwezi ujao.

Simba itatelemka tena uwanjani siku ya jumamosi katika dimba la Mkwakwani Tanga kuwavaa Coastal Union ambao ni wababe wa Yanga na Azam, vigogo hivyo vyote vililala kwa Wagosi hao wa Kaya.

Yanga ilifungwa mabao 2-0 wakati Azam ilichapwa 1-0 na kuweza kutibua kasi yao ya kuelekea kwenye ubingwa

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC