Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MAONI: SIMBA ITANUFAIKA NA VIPOLO VYA YANGA NA AZAM

Na Prince Hoza

Kwanza ningeanza kwa kuzipongeza timu za Yanga na Azam kwa ushindi wao walioupata katika michuano ya kimataifa na kuiwakilisha vema nchi yetu ya Tanzania.

Yanga iliifungasha virago APR ya Rwanda kwa kuifunga jumla ya mabao 3-2, Azam nayo imeitoa Bidvest Wits ya Afrika Kusini kwa jumla ya mabao 7-3, sasa timu hizo zimetinga raundi ya pili.

Kwenye mada yangu ya leo naizungumzia klabu ya Simba yenye maskani yake mtaa wa Msimbazi Kariakoo jijini Dar es Salaam, hivi karibuni uongozi wa Simba ulitishia kutoingiza timu uwanjani mpaka pale Yanga na Azam zitakapocheza mechi zake za ligi ili kusiwepo na vipolo.

Yanga na Azam wana vipolo vya mechi tatu dhidi ya Simba ambayo hadi sasa imecheza mechi 24 huku Yanga na Azam zimecheza mechi 21, Simba wametishia kugoma na wakiitaka TFF kuzipangia mechi Yanga na Azam ili zikamilishe vipolo vyao.

Yanga na Azam zimeshindwa kucheza mechi zake za ligi kwakuwa zibabanwa na ratiba ya michuano ya kimataifa, Yanga inawakilisha taifa ikishiriki michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika wakati Azam yenyewe inashiriki kombe la shirikisho barani Afrika.

Lakini Simba hawataki kusikia hilo, wanataka kuona Yanga na Azam zinacheza mechi zake ili mwisho wa ligi kusiwepo na suala la kupanga matokeo, malalamiko ya Simba mimi nayaunga mkono kwani kwa upande mwingine yanaibeba Simba.

Simba imekuwa ikipata matokeo mazuri katika mechi zake za ligi huku Yanga na Azam zikisaliwa na vipolo, vipolo vya Yanga na Azam vinaweza kuisaidia Simba kwani hadi sasa inaongoza ligi tena ikiwa na pointi 57 huku hao Yanga na Azam wanapointi 50.

Uwiano wa magoli ya kufunga na kufungwa ndiyo yanazigawa timu hizo mbili, Simba wanataka kugomea ligi na TFF imesema wataihsusha daraja iwapo itathubutu kufanya hivyo.

Simba inaweza kubebwa na vipolo vya Yanga na Azam kwani timu hizo zinaweza kukutana na changamoto ya ushindani kutoka kwa timu zinazoshiriki ligi hiyo, kuna uwezekano mkubwa Yanga ikakutana na timu zinazopigania kubaki ligi kuu hivyo zikawapa ushindani ama kutokukubali kufungwa na kulazimisha sare ambayo itaisaidia sana Simba.

Pia Yanga inaweza kupoteza kwani hakuna timu ambayo haijawahi kufungwa, Simba ina mtaji mkubwa wa pointi wakati Yanga na Azam zina mtaji wa vipolo ambavyo vinaweza kuchacha.

Kama Wanasimba watakuwa makini na matokeo mazuri inayopata bila kuwaangalia Yanga na Azam inaweza kunufaika, lakini kama itachungulia wenzake basi inaweza kujikuta inaambulia patupu.

Kiukweli kabisa Watanzania tunapaswa kuwa kitu kimoja ili kuziunga mkono Yanga na Azam ambao ndio wawakilishi wetu pekee katika michuano ya kimataifa.

Endapo Yanga na Azam zitapewa muda wa kujiandaa basi zinaweza kufanya vizuri, Yanga itakutana na miamba ya Misri National Al Ahly wakati Azam itakutana na miamba ya Tunisia Esperance, Simba tumieni nafasi hii mnayoipata ya kutangulia kucheza kwani inaweza kuwanufaisha mwisho wa ligi.

Mwandishi wa makala hii ni mchambuzi wa soka hapa nchini na anapatikana kwa namba 0652626627.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC