Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MAONI: KIMAHESABU YANGA NA AZAM ZIMESHATOLEWA CAF

Na Prince Hoza, DAR ES SALAAM

KWANZA naanza na hii ya kutofanyika kwa mchezo wa kufuzu fainali za mataifa Afrika kati ya Tanzania na Chad ambao ulikuwa uchezwe leo Machi 28 uwanja wa Taifa Dar es Salaam.

Ina maana CAF itaifungia Chad na kuitoza faini, vilevile matokeo yake yote kufutwa, hivyo Tanzania itabakiwa na pointi yake moja, huku Misri ikiendelea kuwa kinara na pointi nne.

Itakuwa ngumu tena Tanzania kufuzu kwenye kundi G kwani limesaliwa na timu tatu na litakosa nafasi ya kutoa 'Best Rooser' na kuinyima nafasi nchi yetu kufuzu kwa mara ya pili fainali hizo za Afrika zitakazofanyika mwakani nchini Gabon.

WAWAKILISHI WENGINE WA TANZANIA NAO SHAKANI.

Tanzania ina wawakilishi wengine wawili katika mashindano ya vilabu barani Afrika, wawakilishi hao ni Yanga Sc na Azam Fc.

Yanga Sc inashiriki michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika wakati Azam Fc inashiriki michuano ya kombe la shirikisho barani Afrika, timu zote hizo zimetinga raundi ya pili na zote zinakabiliwa na mechi ngumu mwanzoni mwa mwezi ujao.

Yanga itaanza na miamba ya Kaskazini, Al Ahly (National) mchezo wa kwanza ukianzia Dar es Salaam na marudiano yakifanyika Cairo, Yanga na Al Ahly watacheza April 9 na marudiano April 19 au 20.

Wakati Azam Fc wataikaribisha Esperance ya Tunisia mchezo wa kwanza ukifanyika Azam Complex na marudiano jijini Tunis, mechi ya Azam na Esperance zitachezwa April 10 na marudiano April 21.

Lakini nina wasiwasi na timu hizo za Tanzania, kwanza zinakutana na miamba ya Afrika, Al Ahly na Esperance ni washindani wa kweli katika michuano yote ya Afrika na zimekuwa zikipambana haswa kila michuano hiyo inapofanyika, Al Ahly na Esperance lazima zitafika hatua ya makundi.

Timu za Tanzania mara yake ya mwisho kucheza hatua ya makundi ni mwaka 2003 wakati Simba Sc ilipofanya hivyo.

Lakini ufinyu wa ratiba ya ligi kuu ndio inayopelekea hofu ya kutolewa kwa wawakilishi hao wote wawili, Yanga itapata siku mbili tu kujiandaa na Al Ahly kwani inabanwa na ratiba ya ligi kuu bara na kombe la FA.

Yanga na Azam zote zimepangiwa mechi nne za mashindano ya ndani, tatu za ligi kuu na moja kombe la FA, mechi hizo wataanza kuzicheza mwishoni nwa wiki hii.

Yanga wamebanwa na ratiba hivyo hawatapata muda wa kujiandaa dhidi ya Al Ahly ambao wao watacheza mchezo mmoja tu wa ligi ya kwao Misri kabla kuivaa Yanga, hakuna asiyetambua uwezo wa Waarabu hao wa kaskazini, Azam nao wamebanwa na ufinyu wa ratiba yao ya ligi.

Ili timu hizo mbili zijiandae angalau TFF na Bodi ya ligi zingeangalia utaifa zaidi na kuzipa muda wa kujiandaa na mapambano hayo, kama Watanzania tunataka mafanikio katika michuano ya kimataifa tuondoe ushabiki na kuziunga mkono Yanga na Azam, ushabiki utaifanya Tanzania kutokuwa na mwakikishi wowote katika mashindano ya CAF isitoshe timu yetu ya taifa imeshapotezewa mwelekeo na Chad.

Tukutane wiki ijayo, nawatakia kila la kheri Pasaka njema.

Mwandishi wa makala hii ni mchambuzi wa soka hapa nchini na anapatikana kwa namba 0652626627.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC