MAJALIWA MGENI RASMI STARS VS CHAD JIMATATU TAIFA, KIINGILIO MKONO WAKO

Na Mrisho Hassan, DAR ES SALAAM

Waziri mkuu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania mhe Majaliwa Kassim Majaliwa anatazamiwa kuwa mgeni rasmi katika mchezo wa mchujo mataifa Afrika kati ya Taifa Stars na Chad uwanja waTaifa Dar es Salaam.

Mchezo wa marudiano utakaopigwa jumatatu, unatazamiwa kuwa mkali na wa kusisimua kutokana na matokeo ya mchezo wa kwanza ambapo Stars ilishinda 1-0 na kujiweka katika mazingira mazuri ya kufuzu fainali hizo zitakazofanyika mwakani Gabon. 

Shirikisho la kandanda nchini TFF limetangaza viingilio vya mchezo huo ambapo shilingi 5000 tu sawa na mkono mmoja wa mwanadamu wenye vidole vitano vinatosha kukupeleka Taifa kuziona Stars na Chad.

Katika mchezo huo wa marudiano Taifa Stars inahitaji ushindi ili ijiwekee mazingira mazuri ya kufuzu kwani Misri na Nigeria zilitoka sare ya 1-1 katika mchezo wao uliofanyika jumatano iliyopita.

Waziri mkuu mhe Majaliwa Kasimu Majaliwa, atakuwa mgeni rasmi jumatatu

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

STAA WETU: JEREMIA JUMA MTOTO WA JUMA MGUNDA ALIYEIKACHA SIMBA NA KUENDELEA NA UASKARI