Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MAONI: NITASHANGAA SANA KAMA TFF ITAZIACHIA GEITA GOLD NA POLISI TABORA BILA KUZIFUNGIA

Na Prince Hoza

NI dhahili kabisa matokeo yamepangwa, hakuna ligi yenye ushindani mkubwa kama ligi Daraja la kwanza Tanzania bara (FDL).
Lakini cha kushangaza timu zinapigwa 8-0 na nyingine 7-0 halafu mechi za mwisho ambazo zinaamua nani apande ligi kuu bara, Geita Gold Mine inayonolewa na nchezaji wa zamani na kocha msaidizi wa Simba Sc Seleman Matola iliitungua JKT Kanembwa ya Kigoma mabao 8-0.
Huo ulikuwa mchezo wa mwisho ambao umeiwezesha Geita Gold kupanda ligi kuu bara, wakati Geita ikiichapa Kanembwa, Polisi Tabora nayo ikaichapa JKT Orjolo mabao 7-0.
Polisi nayo ilihitaji ushindi mkubwa kama huo ili iweze kuungana na Ruvu Shooting na Aftican Lyon ambazo tayari zimeshapanda ligi kuu bara.
Ushindi mkubwa wa Geita Gold na ule wa Polisi Tabora si kwamba naupinga kwa chuki binafsi, hapana, Geita Gold naifahamu sana ni timu yenye uwezo mkubwa wa kusakata kandanda na inao uwezo wa kushinda mabao mengi kama hayo.
Si mara ya kwanza klabu za ligi kuu kukubali vipigo kama hivyo, tulishuhudia Coastal Union ikifungwa mabao 8-0 na Yanga msimu uliopita, lakini sote tuliridhika na kipigo hicho.
Hakuna shaka ypoyote kwenye ushindi huo wa Yanga, tuliamini kiwango chao kilistahili kupata matokeo hayo, Geita Gold nayo naiheshimu sana.
Inacheza vizuri na iliwahi kuifunga Simba mabao 3-1 mchezo wa kirafiki, lakini kinachonisikitisha ni kupata ushindi mkubwa kwenye mchezo wa mwisho ambao walihitaji mabao kama hayo ili wapande ligi kuu.
Kwa vyovyote TFF itapinga kwa nguvu zote matokeo hayo na njia nzuri ya kufanya ili kuondoa mizozo mechi hizo mbili zote zirudiwe katika viwanja vingine.
Ama ikibainika kweli wamepanga matokeo basi hakuna shaka timu hizo zote nne zilizopanga matokeo zishushwe daraja, nitashangaa sana kama TFF itaziachia Geita na Polisi na kubariki matokeo yao kwani naamini kabisa ligi Daraja la kwanza ina ushindani mkubwa kuliko hata wa ligi kuu bara.
TUONANE WIKI IJAYO

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC