Ruka hadi kwenye maudhui makuu

NI SIMBA AU YANGA NANI ATACHEKA BAADA YA DAKIKA 90

Na Alex Jonas

Ni pambano la kihistoria linatarajia kupigwa jioni ya leo katika uwanja wa Taifa Dar es salaam ambapo miamba ya soka nchini Simba na Yanga itakapepetuana.

Timu zote zimejiandaa kuelekea mchezo huo ambapo kila moja iliweka kambi nje ya jiji kwa ajili ya kujiandaa na mchezo huo.

Simba ambao ni vinara wa ligi hiyo wakiwa na pointi 45 waliweka kambi yao mjini Morogoro, Simba ina kumbukumbu nzuri ya kushinda mechi sita mfululizo.

Kikosi cha Simba kinachonolewa  na Jackson Mayanja kina hali nzuri ya kuibuka na ushindi katika mchezo huo, Simba inajivunia washambuliaji wake wanne Hamisi Kiiza, Ibrahim Ajibu, Danny Lyanga na Mwinyi Kazimoti.

Bila shaka nashabiki wake wanajipa matumaini ya kuondoka na ushindi mbele ya Yanga ambao ni mabingwa watetezi wa ligi kuu bara.

Yanga wao waliweka kambi yao Pemba ambapo wana kumbukumbu napo kwani katika mchezo wao wa kwanza na Simba walikaa eneo hilo na wakashinda mabao 2-0.

Hivyo mashabiki wake wanaaminj leo watatoka na ushindi, Yanga inayonolewa na Mholanzi Hans Pluijm itawategemea zaidi Donald Ngoma, Amissi Tambwe, Haruna Niyonzima na Thabani Kamusoko.

Bila shaka mchezo huo utakuwa mkali na wa kuvutia, wakati miamba hiyo ikiumana Taifa, jijini Mbeya matajiri wa bongo Azam Fc wana kibarua kigumu watakapocheza na wagonga nyundo wa Mbeya City

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC