Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MAONI: SIMBA IACHE VISINGIZIO, IKUBALI ILIZIDIWA MBINU NA YANGA

Na Prince Hoza

Simba Sc juzi jumamosi ilikubali kichapo cha mabao 2-0 toka kwa mahasimu wao Yanga Sc katika uwanja wa Taifa Dar es Salaam mchezo wa ligi kuu bara.

Jumla Simba imefungwa na Yanga mara mbili ndani ya msimu huu, kuelekea katika mchezo huo, timu zote zilijiandaa vema.

Simba ndiyo iliyokuwa katika morali ya hali ya juu kwani ilikuwa ikifanya vizuri katika mechi, ushindi mfululizo ilioupata dhidi ya Kagera Sugar 1-0 na Stand United 2-1 zote ikishinda ugenini uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga ziliwapa hamasa kubwa wapenzi na mashabiki wake.

Ushindi huo uliipeleka kileleni Simba na kuwafanya watambe, tofauti na mahasimu zao Yanga ambao waliambulia pointi moja katika mechi zake mbili za ugenini.

Yanga ilifungwa mabao 2-0 na Coastal Union uwanja wa Mkwakwani Tanga, kisha kulazimishwa sare ya mabao 2-2 na Prisons uwanja wa Sokoine Mbeya, matokeo hayo yaliwasononesha sana mashabiki wa timu hiyo na walianzabkuikatia tamaa timu yao.

Licha kwamba Yanga ilichomoza na ushindi wa bao 1-0 ugenini dhidi ya Cercle de Joachim ya Mauritius, lakini ushindi huo haukupokelewa kwa furaha na Wanayanga.

Wanayanga wanafahamu uwezo wa wapinzani wao Cercle kuwa ni wa chini mno hivyo mawazo yao waliyaelekeza kwa Simba, pia hawakuupokea kwa furaha ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya JKT Ruvu.

Hivyo matumaini ya kuifunga Simba yalikuwa madogo, Yanga waliweka kambi yao kisiwani Pemba na hawakutaka kuzungumza na chombo chochote cha habari kuelekea mchezo wake  na Simba.

Simba nao walisikika wakitamba kwenye vyombo vya habari na mara kwa mara viongozi wake kuanzia msemaji wa timu hiyo Hajji Manara na nwenyekiti wa kamati ya usajili Zacharia Hanspoppe walisikika wakitamba na kudai wataifunga Yanga.

Hakuna shabiki wa soka asiyejua makali ya kikosi cha Simba, Hamisi Kiiza "Diego" na Ibrahim Ajibu wamekuwa katika kiwango cha juu na kuzidi kuwatisha mabeki wa Yanga.

Simba iliweka kambi yake mjini Morogoro na kocha wake Jackson Mayanja alikuwa akinukuliwa kwamba vijana wake wako tayari kuimaliza Yanga, lakini viongozi wa Yanga walikaa kimya na hawakutoa ushirikiano wowote.

Lakini ilipotimia siku ya mpambano wenyewe, Februali 20 Simba ilikubali kipigo cha mabao 2-0, goli la kwanza la Yanga lilipatikana kipindi cha kwanza likifungwa na Donald Ngoma na la pili lilipatikana kipindi cha pili likifungwa na Amissi Tambwe.

Mwamuzi wa kati Jonnesia Rukyaa alimtoa mapema beki wa Simba Abdi Banda baada ya kuonyeshwa kadi mbili za manjano, goli la kwanza la Yanga lilitokana na juhudi binafsi za mshambuliaji wa Yanga Donald Ngoma ambaye aliutokea mpira uliokuwa ukirudishwa kwa kipa na Hassan Kessy.

Pia goli la pili lilifungwa na Tambwe lakini zilikuwa juhudi zake binafsi kwani ilipigwa krosi na Geofrey Mwashiuya na kumkuta Tambwe mguuni kwake na kuuweka kimiani.

Tambwe alikaa na Juuko Murushid lakini mbinu zake ndizo zilizopelekea kufunga bao hilo, baada ya mpira kumalizika, viongozi wa Simba pamoja na mashabiki wake walisikika wakimlaumu mwamuzi wa mchezo huo wakidai ndiye aliyesababisha timu yao kufungwa na Yanga.

Simba wanadai timu yao imefungwa kwa sababu Abdi Banda alipewa kadi nyekundu mapema, kwangu hizo ni sababu za kitoto mno, Simba imewahi kuifunga Yanga mara kadhaa huku ikiwa pungufu baada ya mchezaji wake kupewa kadi nyekundu.

Ilishatokea sana kwa Haruna Moshi "Boban" na Victor Costa, sikuwahi kusikia akilalamikiwa mwamuzi baada ya kumalizika mchezo huo, iwejebtena safari hii mwamuzi anaoekana tatizo.

Hizo ni sababu za kitoto, mkubali tu matokeo kwani dhahili Yanga iliwazidi mbinu, mfumo walioutumia Yanga ulitosha kuwapa ushindi wa mabao 2-0, sitaki nielezee kiundani ila Simba mjipange na mkubali matokeo.

Tuonane tena wiki ijayo Inshallah

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...