Ruka hadi kwenye maudhui makuu

#MAONI: TFF IMEHODHI LIGI KWA AZAM

Na Prince Hoza

KITENDO kilichofanywa na shirikisho la kandanda nchini TFF kuiruhusu Azam Fc kwenda Zambia kucheza mechi za kirafiki na kuikacha ligi kiu ya Vodacom Tanzania bata huku ikisababisha kupangua ratiba ya ligi hiyo si cha kuzoeleka hata siku moja.

TFF imefanya kosa kubwa ambalo linaanza kuharibu sifa ya shirikisho hilo pamoja na Bodi yake ya ligi TPLB, Licha kwamba raisi wa shirikisho hilo Jamal Malinzi kuomba radhi lakini bado ni sawa na kazi bure, kwani kosa limeshafanyika.

Bora ruhusa hiyo ingepewa Mwadui Fc au Kagera Sugar sidhani kama wadau wa soka wangelalamika sana, huenda wangelisifu shirikisho hilo kwani timu hizo hazipo kwenye mbio za ubingwa, kitendo cha kuiruhusu Azam Fc kinaonekana kama cha kuipendelea.

Tunafahamu kwamba Azam Fc ni timu inayomilikiwa na bilionea Said Salim Bakhressa ambaye pia ndiye mmiliki wa Azam Tv yeye na familia yake.

Azam Tv ni wadhamini wenza wa ligi kuu bara hivyo ina nguvu ndani ya shirikisho hilo, matajiri hao pia wanadhamini michuano ya kombe la FA.

Azam Fc itakosa mechi mbili za ligi ambazo ilikuwa icheze na Prisons jumamosi iliyopita na Stand United jumatano ijayo, mechi hizo zilipaswa zichezwe pamoja na nyingine ili kusitokee suala la kupanga matokeo.

Azam Fc ipo kwenye mbio za kuwania ubingwa wa bara ikiwa katika nafasi ya pili na pointi zake 39 huku vinara wa ligi hiyo Yanga nao wakiwa na pointi kama hizo 39.

Simba wanakamata nafasi ya tatu na pointi zao 36, kitendo cha Azam kutimkia Zambia kunapelekea kupangwa kwa matokeo kwani imeziacha Yanga na Simba peke yao.

Tayari Yanga imecheza mchezo wake wa 16 na Coastal Union na ikapoteza kwa kifungwa mabao 2-0 katika uwanja wa Mkwakwani Tanga, Azam wameyapata matokeo hayo ya kufungwa kwa Yanga wakiwa mjini Ndola Zambia wanakoshiriki michuano isiyo rasmi.

Kwa vyovyote Azam imeshapata faida kwani mpinzani wake mkuu kwenye mbio hizo Yanga imeshateleza, Azam inahitaji pointi moja tu kuipoka Yanga uongozi.

Madudu ya TFF yanazidi kuendelea kwani kuiruhusu Azam peke yake kwenda kujiandaa na michuano ya kombe la shirikisho barani Afrika ni dhahili kama inaiandaa Azam peke yao wakati Tanzania bara itawakilishwa na timu mbili ikiwemo Yanga.

Yanga itaiwakilisha bara katika michuano mikubwa kuliko yote kwa upande wa vilabu barani Afrika ambayo ni ligi ya mabingwa, hivyo TFF ilipaswa nayo kuipa Yanga muda wa maandalizi kama ilivyofanya kwa Azam.

Yanga ilipata mwaliko nchini Afrika Kusini lakini TFF iliwakatalia, hii inaonyesha kwamba shirikisho hilo limehodhi ligi kuu bara kwa Azam.
TUONANE TENA JUMATATU IJAYO

Call 0652626627

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...