Ruka hadi kwenye maudhui makuu

BEKI AFRICAN SPORTS ATUA SIMBA, MAJWEGA NAYE KIMEELEWEKA

Dirisha dogo la usajili Ligi Kuu Bara limefikia patamu, huku Simba, Yanga na Azam FC zikionekana kuwa kivutio kipindi hiki.

Wakati Yanga bado ikielekeza nguvu za usajili kumnasa mshambuliaji wa Stand United, Elius Maguli, watani wao wa jadi Simba wamemalizana na mlinzi, Novat Lufungo kutoka African Sports ya Tanga.

Wakati Wekundu hao wa Msimbazi wakimalizana na  Lufungo, pia hatua za mwisho kuipata saini ya winga wa Azam FC, Mganda FC Mganda, Brian Majwega.

Habari kutoka ndani ya klabu hiyo ya Msimbazi, zimethibisha usajili wa Lufungo aliyelamba Sh. milioni 10 ili kuvaa jezi nyeupe na nyekundu.


Mazungumzo ya Simba na mchezaji huyo yalikamilika Jumatatu usiku na tayari mchezaji huyo baada ya kumwaga wimo amekwenda kuungana na wenzake waliopiga kambi jijini Zanzibar.

Simba iko Zanzibar kujiandaa na mchezo Ligi Kuu Bara dhidi ya Azam FC utakaochezwa Desemba 12 kwenye Uwanja wa Taifa.

Lufungo, nyota wa zamani Mgambo JKT, amesaini mkataba wa miaka miwili.

“Tumemfuatilia kwa muda mrefu, nashuruku tumemalizana naye salama na ameshakwenda kujiunga na wenzake Zanzibar,” alidokeza mtoa habari ambaye hakutaka jina lake kuandikwa kwenye gazeti kwa kuwa siyo msemaji.
“Huyu ni mchezaji mzuri, anaweza kucheza namba  4, 5 na 6,” aliongeza mtoa habari huyo.

Kwa upande wake, Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara alithibitisha usajili wa mchezaji huyo. Makamu Mwenyekiti wa African Sports, Abdul Bosnia aliliambia gazeti hili kuwa Simba wamekamilisha taratibu zote za kumsajili beki huyo.

“Hatuna shida na Simba, wamekamilisha taratibu zote za usajili. Mambo mengine ni kati ya Simba na mchezaji mwenyewe,” alisema Bosnia.

Katika hatua nyingine, Manara alisema kuwa Majwega ambaye alikuwa akijifua na Simba, anatarajia kurejea nchini wakati wowote akitokea  Uganda.

Endapo Simba itafanikiwa kumsajili Majwega, itafikisha wachezaji wa kimataifa sita ambao wengine ni Hamisi Kiiza, Juuko Murshid kutoka Uganda, Justice Majabvi (Zimbabwe), Emery Nimubona (Burundi) na Vincent Angban wa Ivory Coast.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...