Ruka hadi kwenye maudhui makuu

YANGA KUWAALIKA HEARTS OF OAK YA GHANA KUCHEZA KIRAFIKI

Katika kudhihirisha tambo za msemaji wao, Jerry Muro kwamba 'wao ni wa kimataifa', Yanga wamewaalika mabingwa wa Ligi Kuu ya Ghana, Hearts of Oak, kuja nchini kwa ajili ya mechi ya kirafiki.

Tangu aingie madarakani Januari, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano ya Yanga (Muro) amekuwa akitamba kuwa klabu hiyo ya Jangwani ni ya kimataifa.

Ili kufanya vyema katika michuano ya Klabu Bingwa Afrika mwakani, Yanga wameanza kusaka mechi za kimataifa za kirafiki, safari hii wakikimbilia Ghana alikokuwa anafanyia kazi kocha mkuu wao, Hans van der Pluijm.

Jonas Tiboroha, Katibu Mkuu wa Yanga, aliliambia gazeti hili jijini Dar es Salaam jana kuwa tayari walishapeleka barua ya maombi katika klabu hiyo kongwe inayoshiriki Ligi Kuu ya Ghana na wanaamini wataukubali mwaliko wao.

Tiboroha alisema programu ya benchi la ufundi, imeelekeza timu yao ipate mechi mbili za kirafiki kabla ya ligi haijaendelea na wanaamini watapata mechi hizo ili kukiimarisha zaidi kikosi chao.


"Tunasubiri majibu, ila tunaamini watakubali maombi yetu, hasa kupitia kocha wetu Pluijm (Hans) ambaye aliwahi kufanya kazi Ghana na kufahamiana na viongozi mbalimbali," alisema Tiboroha.

Aliongeza kuwa mshambuliaji wao wa kimataifa kutoka Zimbabwe, Donald Ngoma alirejea nchini juzi wakati kiungo wao Mbrazi Andrey Coutihno naye alitarajiwa kutua jijini jana usiku.

"Kuanzia kesho (leo) Jumatatu mazoezi yetu yatachanganya kwa sababu wachezaji wetu wa kimataifa waliokuwa nje ya nchi wataanza kujinoa na wenzao baada ya kuwa nje ya timu kwa sababu mbalimbali," alisema.

Kiongozi huyo alisema watahakikisha wanatekeleza mapendekezo yote yaliyotolewa na kocha wao ili waiimarishe timu na kufanya vizuri katika mashindano yote ya kimataifa watakayochuana mwakani.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC