Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MAKALA: UNAMKUBUKA LUCAS NKONDOLA? MCHEZAJI ALIYEWEZA KUCHEZA NAFASI NYINGI UWANJANI

MICHUANO ya mataifa Afrika mashariki na kati maarufu kombe la Chalenji inaendelea kushika kasi nchini Ethiopia katika miji ya Adis Ababa na Awassa City, Tanzania inawakilishwa na timu za taifa mbili Kilimanjaro Stars kwa upande wa bara na Zanzibar Heroes kwa upande wa Zanzibar.

Kilimanjaro Stars ilikuwa timu ya kwanza kujikatia tiketi ya kucheza robo fainali baada ya kushinda mechi zake mbili mfululizo za mwanzo, ikumbukwe michuano ya Chalenji ndiyo michuano mikubwa kuliko yote katika ukanda huu wa Afrika mashariki na kati.

Lakini pia ndiyo michuano mikongwe kuliko yote barani Afrika, michuano ya Chalenji inasadikika ilianzishwa mwaka 1924, na kwa mara ya kwanza Tanzania bara baada ya uhuru ilitwaa ubingwa wa michuano hiyo mwaka 1974 ikiwa na kikosi bora kabisa ambacho kinatajwa hakijawahi kutokea.

Kikosi hicho golini alisimama Omari Mahadhi Bin Jabir (sasa marehemu), beki wa kulia alicheza Zaharani Makame, wakati beki wa kushoto alicheza Mohamed Chuma (sasa marehemu), namba nne alicheza Salim Amir wakati sentahafu alisimama Mohamed Bakari 'Tall', namba sita alisimama Jellah Mtagwa, namba saba alicheza Godfrey Nguruko ambaye baadaye kipindi cha pili alitoka na nafasi yake kuchukuliwa na Shiwa Lyambiko.


Namba nane alicheza Sunday Manara 'Computer', wakati sentafowadi alisimama Mwinda Ramadhan, namba kumi alicheza Gibson Sembuli (sasa marehemu) na kumi na moja alicheza winga ya maajabu Lucas Nkondola.

Kati ya wachezaji wachache waliokuwa na uwezo wa kucheza nafasi nyingi wawapo uwanjani ni huyu Lucas Nkondola, kwani alimudu kucheza vyema nafasi ya ulinzi wa kushoto namba tatu, kiungo namba sita na nane pia nafasi ya ushambuliaji wa kushoto namba kumi na moja.

Pamoja na kutamba akiwa na timu ya taifa katika miaka hiyo ya 1970, pia kutokana na umahiri wake wa kusakata soka ameweza kuzichezea timu za Pamba FC ya Mwanza, Sungura FC ya Tabora, Simba SC ya Dar es Salaam, na katika mashindano ya kombe la Taifa Cup, Nkondola aliwahi kuzichezea timu za mikoa mbalimbali.

Aliwahi kuichezea timu ya mkoa ya Mwanza, (Mwanza Heroes), timu ya mkoa wa Shinyanga (Ingenisabo), timu ya mkoa wa Dar es Salaam (Mzizima) na pia kuichezea timu ya taifa ya vijana.

Katika mchezo wa fainali ya mashindano ya Chalenji mwaka 1974, Nkondola ndiye aliyefunga bao pekee kwa upande wa timu ya taifa ya Tanzania bara wakati huo ikijulikana Taifa Stars (sasa Kili Stars), katika dakika ya 25 ya kipindi cha kwanza, kabla ya Uganda Cranes kusawazisha bao hilo katika dakika ya 85.

Pia katika upigaji wa penalti, Nkondola alifunga penalti moja kati ya tano zilizopatikana kwa upande wa Stars siku hiyo, kwa hivi sasa Nkondola anaishi Magomeni jijini Dar es Salaam akijishughurisha na kazi zake binafsi.

Nkondola pia ana mengi ya kukumbukwa alipokuwa na klabu ya Simba ambayo aliichezea kwa mafanikio makubwa, mchezaji huyo hatoweza kusahaulika kutokana na uwezo wake mkubwa aliowahi kuuonyesha

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC