Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KAVUMBAGU AWAITA SIMBA MEZANI

MSHAMBULIAJI wa Azam FC, Didier Kavumbangu amesema amekuwa akisikia sikia tu habari za kutakiwa na Simba SC, lakini hajawahi kuzungumza na kiongozi yeyote wa klabu hiyo.

Akizungumza mjini Addis Ababa, Ethiopia mwishoni mwa wiki, Kavumbangu amesema kwamba na wala klabu yake, Azam FC haijawahi kumpa taarifa zozote za kuhamishwa kwa mkopo.

“Nasikia Simba SC wananitaka kwa mkopo. Nasikia sikia tu, lakini sijawahi kuambiwa na klabu yangu, wala Simba SC hawajawahi kunifuata,”amesema mshambuliaji huyo wa zamani wa Yanga SC na TP Mazembe ya DRC.

Alipoulizwa iwapo Simba SC wana nia kweli ya kumchukua, Kavumbangu anayechezea Burundi kwenye Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge amesema; “Siwezi kuzungumza hadi Simba wakinifuata ndiyo nitawajibu, lakini kwa sasa mimi ni mchezaji wa Azam FC na nina Mkataba,”amesema.

Rais wa Simba SC, Evans Elieza Aveva mwishoni mwa wiki alisema kwamba hawajawahi kufanya mazungumzo na Kavumbangu, lakini wanasikia nao kwamba Azam FC inataka kumuacha.


“Kwa sasa hatuwezi kuzungumza chochote, hadi hao Azam FC wamuache, labda tunaweza kuzungumza, tunakiri ni mchezaji mzuri,”alisema.
Kavumbangu alijiunga na Azam FC msimu uliopita kutoka Yanga SC na alikuwa na msimu mzuri wa kwanza chini ya kocha Mcameroon, Joseph Marius Omog akicheza na kufunga mabao, kiasi cha kuwafurahisha hadi wamiliki wa timu, akaongezwa Mkataba wa mwaka mmoja.

Hata hivyo, baada ya kurejeshwa kwa Muingereza Stewart John Hall, Kavumbangu amepoteza nafasi kwenye kikosi cha kwanza cha timu hiyo ya Alhaj Sheikh Said Salim Awadh Bakhresa na familia yake.

Lakini mechi tatu zilizopita za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Kavumbangu alianzishwa zote na akafunga katika kilamechi na kutimiza jumla ya mabao 19 ya kufunga katika mechi 46 za mashindano yote alizocheza.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC