Ruka hadi kwenye maudhui makuu

ERICK MAJALIWA: Alisababisha mgogoro mkubwa wa kiuongozi Simba, inadaiwa ni mtoto wa waziri mkuu



HISTORIA imeandikwa katika soka la Tanzania hasa baada ya Rais wa

jamhuri ya muungano Mhe John Pombe Magufuli kumteua mbunge wa

Ruangwa mkoani Lindi Majaliwa Kasimu Majaliwa kuwa Waziri mkuu wa

11 wa Tanzania.

Uteuzi huo ulipokelewa kwa hisia tofauti toka kwa Watanzania, wapo

walioshangazwa na uteuzi huo ambao waliamini huenda lingetangazwa

jina kubwa lililozoeleka masikio mwao, na wengine walishangaa tu

kuona Naibu waziri TAMISEMI wa serikali ya Awamu ya nne anakuwa

waziri mkuu serikali ya Awamu ya tano.



Pia uteuzi huo uliwashangaza wanamichezo, hawakutarajia kabisa

kusikia mwanamichezo mwenzao anateuliwa na Rais kuwa waziri mkuu,

mhe Majaliwa ni kocha wa soka mwenye leseni B inayotambulika na

CAF, Majaliwa pia ni kocha wa timu ya Bunge FC huku pia akikinoa

kikosi cha Wabunge wanaoshabikia Simba SC.

Kwa mashabiki wa Simba walilipuka furaha kwani Mhe Majaliwa ni

Simba mwenzao tena damu, lakini kikubwa zaidi Mhe Majaliwa ni baba

wa kiungo wa zamani wa Simba, Erick Majaliwa.

Wakati anateuliwa tu rais Magufuli, kwenye mitandao ya kijamii

ziliibuka taarifa zake kuwa ni baba wa kumzaa Erick Majaliwa, Erick

aliwahi kuichezea imba mwanzoni mwa miaka ya 2000 ingawa hakudumu

sana , mchezaji huyo alisajiliwa na Simba baada ya kumuona akicheza

vizuri kwenye timu ya shule ya sekondari ya Makongo iliyokuwa

ikisimamiwa na Kanali mstaafu Idd Kipingu, Makongo ilisifika kwa

kutoa wachezaji mbalimbali hapa nchini.

Erick alikuwa mchezaji mzuri mwenye nidhamu na uwezo wa kucheza

nafasi tofauti, nyota huyo wa zamani wa Simba hakuwahi kutamba sana

lakini aliweza kujizolea sifa kemkem, Erick aliwavutia wengi

kutokana na kiwango chake licha ya kukutana na changamoto ya namba.

Wakati huo Simba ilikuwa na mastaa lukuki ambao walisababisha nyota

huyo kushindwa kuunguruma na kuishia benchi, Majaliwa asingeweza

kupata namba mbele ya Haruna Moshi 'Boban' hivyo uongozi wa Simba

uliamua kumtoa bure kwa timu ya Al Shaab Hadramaut ya Yemen.

Majaliwa aliungana na kocha wake Jamhuri Kihwelu 'Julio' ambaye

naye aliwahi kuichezea Simba na baadaye kuifundisha akiwa kama

kocha msaidizi, inadaiwa aliyekuwa katibu mkuu wa Simba Mwina Seif

Kaduguda ndiye aliyemwidhinishia kujiunga bure na timu hiyo ya

Yemen.
Waziri mkuu Mhe Kasimu Majaliwa akikabidhi bendera kwa timu ya vijana

Timu hiyo ya Yemen iliyokuwa ikishiriki ligi kuu ilikusanya

wachezaji lukuki kutoka Tanzania ambao wote walipatiwa vibali vya

uhamisho, wachezaji wengine walioungana na Majaliwa ni Monja

Liseki, John Njama na Omari Changa (sasa marehemu).

Baadaye viongozi wa Simba waliingia katika mzozo mkubwa kufuatia

mchezaji huyo kuruhusiwa bure bila klabu kuingiza kiasi chochote,

Kaduguda na mwenyekiti wa Simba Hassan Dalali walishutumiana

waziwazi, huenda Erick Majaliwa kwa sasa anaangukia kwenye neema

nyingine baada ya ile ya kuichezea Simba kama ni kweli mtoto wa

waziri mkuu

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC