Ruka hadi kwenye maudhui makuu

NGOMA, KIIZA WATISHA KWA MABAO LIGI KUU BARA 2015/16

Yanga ilishinda 2-0 katika mechi yake ya ufunguzi wa msimu Jumapili iliyopita dhidi ya Coastal Union kupitia mabao ya Mzimbabwe, Donald Ngoma, na mzawa Simon Msuva, wakati katika mechi yao ya pili mabingwa hao walishinda 3-0 dhidi ya Tanzania Prisons kupitia magoli ya beki wa Rwanda, Mbuyu Twite, Mrundi Amisi Tambwe na Mzimbabwe, Donald Ngoma.

Mahasimu wao, Simba, kufikia sasa wamefunga jumla ya magoli matatu, mawili yakifungwa na Mganda Hamis Kiiza na moja Mzimbabwe, Justice Majabvi. Wekundu wa Msimbazi walishinda 1-0 dhidi ya African Sports katika mechi ya ufunguzi kwenye Uwanja wa Mkwakwani, Tanga kabla ya kuilaza Mgambo Shooting 2-0 juzi kwenye uwanja huohuo.

Washindi wa pili wa msimu uliopita, Azam FC, kufikia sasa baada ya mechi mbili za ligi hiyo ya juu zaidi nchini, wamefunga jumla ya magoli manne, mawili ya nyota wa kigeni Muivory Coast, Kipre Tchetche na Mkenya, Allan Wanga huku mengi mawili yakifungwa na Farid Mussa na Frank Domayo. Azam ilishinda 2-1 dhidi ya Prisons kwenye Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam kabla ya juzi kuilaza Stand United 2-0 kwenye Uwanja wa Kambarage, Shinyanga.

Mabao 17 ya juzi ni ongezeko la mabao sita zaidi ya yaliyofungwa katika raundi ya kwanza msimu huu na mawili zaidi ya ilivyokuwa raundi ya pili msimu uliopita.


Mshambuliaji Donald Ngoma wa Yanga, ana mabao mawili kama mwenzake Hamisi Kiiza wa Simba

Katika jumla ya mabao 28 yaliyofungwa katika raundi mbili za kwanza msimu huu, mabao 9 yamefungwa na wageni, sawa na asilimia 32 ya mabao yote. Ligi Kuu ya Bara msimu huu ina jumla ya wachezaji 29 wa kigeni. Simba, Yanga na Azam zinao nyota wa kigeni 7 kila moja, Coastal Union wanne, Stand United (2), Mbeya City (1) na African Sports mmoja. 

Mabao 11 ya raundi ya pili juzi yalifungwa na timu mwenyeji huku wachezaji Miraji Athuman (Toto), Donald Ngoma (Yanga), Hamis Kiiza (Simba) na Atupele Green (Ndanda) wakifunga bao moja na kufikisha mabao mawili kila mmoja msimu huu baada ya kutupia pia bao moja-moja katika mechi za raundi ya kwanza Jumamosi na Jumapili.

Mabao mawili yalifungwa kwa penalti na Ngoma na Themi Felix wa Mbeya City wakati beki wa Prisons James Josephat aliweka rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza kutolewa kwa kadi nyekundu msimu huu baada ya kumkwatua winga, Simon Msuva na kusababisha penalti.  Yanga imecheza mechi mbili bila wachezaji wake kuonyeshwa kadi hata moja ya njano.  Kiungo Nizar Khalfan wa Mwadui FC ndiye ameweka rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza kukosa penalti baada ya kushindwa kufunga kwa ‘tuta’ katika mechi yao ya kwanza waliyolala 1-0 dhidi ya Toto Africans jijini Mwanza Jumamosi.

Matokeo ya mechi za juzi yalikuwa Yanga 3-0 Prisons, Majimaji 1-0 Kagera, Mbeya City 3-0 JKT Ruvu, Ndanda 1-0 Coastal, Mwadui 2-0 A/Sports, Stand 0-2 Azam, Toto 1-2 Mtibwa, na Mgambo 0-2 Simba.
Katika raundi ya pili ya VPL msimu uliopita (timu zilikuwa 14) mabao 15 yalifungwa (sita yalifungwa na timu zilizocheza ugenini, sawa na msimu huu).

Matokeo ya raundi hiyo msimu uliopita yalikuwa Simba 1-1 Police Moro, Mtibwa 3-1 Ndanda, Azam 2-0 Ruvu Shooting, Mbeya City 1-0 Coastal, Mgambo 0-1 Stand, JKT Ruvu 0-2 Kagera, na Yanga 2-1 Prisons.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC