Ruka hadi kwenye maudhui makuu

CHELSEA YAZINDUKA NA KUPIGA MTU 4-0 ULAYA, BARCA YASHIKWA SHATI

CHELSEA inayovurunda katika Ligi Kuu ya England, usiku huu imefufua makali na kuitandika mabao 4-0 Maccabi Tel Aviv ya Israel katika mchezo wa Kundi G Ligi ya Mabingwa Ulaya Uwanja wa Stamford Bridge, London.
Mabao ya The Blues inayofundishwa na Mreno Jose Mourinho yamefungwa na Willian Borges Da Silva dakika ya 15, Oscar dos Santos Emboaba Junior kwa penalti dakika ya 49, Diego Da Silva Costa dakika ya 58 na Cesc Fabregas dakika ya 78.

Mchezo mwingine wa kundi hilo, Dynamo Kyiv imelazimishwa sare ya 2-2 na FC Porto Uwanja wa Olimpiki, Mabao ya Dynamo yamefungwa na Oleg Gusev dakika ya 20 na Vitaliy Buyalsky dakika ya 89 wakati ya Porto yamefungwa na Vincent Aboubakar dakika ya 23 na 81.
Barcelona superstar Lionel Messi was one of the first players to congratulate Suarez after his goal against the Italian outfit

Nyota wa Barcelona, Lionel Messi akimpongeza Suarez baada ya kufunga bao la kuongoza PICHA ZAIDI
Arsenal imechapwa mabao 2-1 na Dinamo Zagreb katika mchezo wa Kundi H, mabao ya wenyeji yakifungwa na Alex Oxlade-Chamberlain aliyejifunga dakika ya 24 na Junior Fernandes dakika ya 58, wakati The Gunners bao lao lilifungwa na Theo Walcott dakika ya 79 Uwanja wa Maksimir.


Mchezo mwingine wa kundi hilo, Bayern Munich imeshinda 3-0 ugenini dhidi ya Olympiakos, mabao ya Thomas Muller dakika ya 52 na 90+2 kwa penalti, lingine likifungwa na Mario Gotze dakika ya 89 Uwanja wa Georgios Karaiskakis.

Kundi E; Bayer 04 Leverkusen imeshinda 4-1 dhidi ya BATE Borisov, mabao yake yakifungwa na Admir Mehmedi dakika ya nne, Hakan Calhanoglu dakika ya 47, Javier Hernandez ‘Chicharito’ dakika ya 58 na Hakan Calhanoglu kwa penalti dakika ya 75, wakati la BATE limefungwa na Nemanja Milunovic dakika ya 13 Uwanja wa BayArena.

Mchezo mwingine wa kundi hilo, mabingwa watetezi, FC Barcelona wamelazimishwa sare ya 1-1 na AS Roma Uwanja wa Olimpico. Luis Suarez alianza kuifungia Barca dakika ya 21 kabla ya Alessandro Florenzi kuisawazishia Roma dakika ya 31.

Kundi H; Valencia CF imechapwa 3-2 na Zenit St Petersburg Uwanja wa Mestalla, mabao yake yakifungwa na Axel Witsel aliyejifunga dakika ya 54 na Andre Filipe Tavares Gomes dakika ya 73, huku mabao ya washindi yakifungwa na Givanildo Vieira de Souza dakika ya tisa na 44 na Witsel aliyesawazisha makosa yake dakika ya 76.
Mchezo mwingine wa kundi hilo, KAA Gent imelazimishwa sare ya 1-1 na Lyon bao lao likifungwa na Danijel Milicevic dakika ya 68 baada ya Christophe Jallet kuanza kuifungia Lyon dakika ya 58 Uwanja wa Ghelamco.

MATOKEO MECHI ZA LIGI YA MABINGWA USIKU HUU

Chelsea 4-0 Maccabi Tel Aviv
Dinamo Zagreb 2-1 Arsenal
Roma 1-1 Barcelona
Olympiakos 0-3 FC Bayern Munchen
Valencia CF 2-3 Zenit St Petersburg
KAA Gent 1-1 Lyon
Dynamo Kyiv 2-2 FC Porto
Bayer 04 Leverkusen 4-1 BATE Borisov
Mshambuliaji wa Chelsea, Costa akishangilia na mchezaji mwenzake, Oscar baada ya kufunga bao la tatu

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC