Ruka hadi kwenye maudhui makuu

HALL AIKUBALI MUZIKI WA YANGA SC

Baada ya kuikosa Ngao Jamii kwa mara ya pili mfululizo mbele ya Yanga, Kocha Mkuu wa Azam FC, Muingereza Stewart Hall, amekiri kuwa vijana hao wa Mholanzi Hans van der Pluijm waliwazidi uwezo katika mechi hiyo iliyopigwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam juzi.

Hall pia alifafanua kuwa timu yake haikuwa vizuri katika dakika 20 za mwisho na walionekana wako tayari kusubiri kufika hatua ya matuta jambo ambalo halikuwa sahihi.

Kocha huyo alisema mechi hiyo ilikuwa ngumu na yenye ushindani kwa timu zote mbili hali iliyosababisha kumalizika dakika 90 za kawaida bila ya kufungana.

"Katika soka lazima uwe fiti kila upande, kama hauko fiti labda ukacheze mpira wa kikapu," alisema Hall.
Aliongeza kuwa mashabiki wa Yanga walisaidia pia kuipa ushindi timu yao, jambo lililowafanya wachezaji wao kujiona kama wako 12 kitu ambacho timu yake inakikosa.

"Nataka kusema jambo moja, mashabiki wa Yanga walifanya vizuri sana kuisaidia timu yao kwa kuishangilia, kitu ambacho sisi hatuna, kuna wakati unaona kama wako 12 uwanjani, au kama unacheza mechi nyingine, walikuwa wakiwashangilia kila walipokuwa na mpira na walituzomea pale tulipokuwa tunawashambulia," Hall aliongeza.


Pluijm alimjibu Hall kwa kueleza kuwa hiyo haikuwa sababu mojawapo ya yeye kufungwa kwa sababu kikosi chake kilikuwa pia kinashangiliwa na mashabiki wa Simba waliofika uwanjani hapo.

Mholanzi huyo alisema ushindi ambao timu yake iliupata juzi ni wa kulipa 'kisasi' na ulitokana na wachezaji wake kucheza katika kiwango cha juu ili kutimiza malengo yao.

Yanga ambao ni mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara waliibuka na ubingwa wa Ngao ya Jamii baada ya kuifunga Azam kwa penalti 8-7 kufuatia timu hizo mbili kutoka suluhu ndani ya dakika 90 za kawaida.

Alisema mchezo huo ulikuwa mgumu na wenye ushindani lakini amefurahi timu yake ilifanikiwa kuibuka na ushindi na hatimaye kuanza vema msimu mpya wa ligi wa mwaka 2015/ 2016.

Pluijm alisema kila timu ilitengeneza mashambulizi kwa kiwango kinacholingana lakini akaipongeza zaidi safu yake ya ulinzi kwa kuwa makini ukilinganisha na mechi iliyopita.

"Katika soka kila siku kuna ushindani, na kila nafasi unayopata unatakiwa uitumie vizuri, tulitengeneza nafasi na wao walitengeneza nafasi pia, ulikuwa ni 50 kwa 50, hakuna ambaye alizidiwa moja kwa moja, hata ukiangalia kwenye mechi za Ligi Kuu ya England utashuhudia kuna baadhi ya mechi timu zinapanda na kushuka, ni hali ya kawaida kwenye mpira,"alisema kocha huyo ambaye timu yake iliondolewa na Azam katika hatua ya robo fainali kwenye mashindano ya Kombe la Kagame hivi karibuni.

Hata hivyo, Pluijm alisema kuwa kikosi chake hakikuwa kwenye kiwango cha juu katika dakika 90 za kawaida na kwamba hiyo ndiyo soka lakini amefurahishwa na ushindi walioupata ambao umewapa faraja.

Baada ya mechi hiyo, tayari msimu mpya umeanza na katika mechi ya ufunguzi Septemba 12, mwaka huu, Azam itaikaribisha Tanzania Prisons kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi jijini Dar es Salaam wakati Simba ikianzia ugenini Tanga kwa kuvaana na African Sports huku siku inayofuata Yanga yenyewe ikianza kutetea ubingwa wake kwa kucheza dhidi ya Coastal Union kutoka Tanga.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC