Ruka hadi kwenye maudhui makuu

YANGA YAMALIZANA NA STRAIKA LA PLATINUM YA ZIMBABWE

Katika kuhakikisha inafanya vizuri katika msimu ujao wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara pamoja na mashindano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, uongozi wa Yanga umesema umemalizana na mshambuliaji wa Platinum FC ya Zimbabwe, Donald Ngoma, baada ya kukubaliana kusaini mkataba wa miaka miwili.

Kwa mujibu wa habari zilizopatikana kutoka ndani ya uongozi wa Yanga tayari wamekamilisha mazungumzo na mchezaji huyo na anatarajiwa kutua nchini mapema mwezi ujao kumaliza taratibu zilizobaki na kisha kuungana na kikosi cha mabingwa hao wa Bara ambacho kitaanza mazoezi Juni 8, mwaka huu.

Chanzo hicho kiliendelea kueleza kuwa wanaamini uwezo wa mshambuliaji huyo wa timu ya Taifa ya Zimbabwe utasaidia kuimarisha safu ya ushambuliaji baada ya Mrisho Ngasa kuondoka.

"Hapa ninavyozungumza na wewe huyo mchezaji ni mali ya Yanga tayari, tumeshamalizana naye, tumempa mkataba wa miaka miwili," alisema kiongozi huyo wa juu wa Yanga.


Aliongeza kuwa usajili wa mwaka huu utafanyika kwa mapendekezo ya kocha na hakutakuwa na mchezaji atakayeletwa na kiongozi au mwanachama yeyote wa timu hiyo.

"Tuliahidi kuiboresha Yanga, tutafanya kila kitu kisasa kulingana na taratibu zinazostahili, kwa upande wa usajili, mwalimu ndiye anajua ubora wa timu na mapungufu yaliyoko, yeye ndiye atasema nani asajiliwe au aachwe," aliongeza.

Ngoma jana jioni alitarajiwa kuiongoza safu ya ushambuliaji ya Zimbabwe dhidi ya Mauritius kwenye mashindano ya Kombe la Cosafa yanayofanyika Afrika Kusini kwa kushirikisha timu mbalimbali za Ukanda wa Kusini mwa Afrika, Tanzania ikiwa mojawapo kama nchi alikwa.

Mbali na nyota huyo, tayari Yanga imeshamnasa Mwinyi Haji Mngwali wa KMKM ya Zanzibar ambaye kwa sasa ameitwa katika kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) kilichoko Afrika Kusini.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...