Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Nooij: Stars fiti kuivaa Swaziland leo.

Timu ya Soka ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars), leo inatarajiwa kushuka katika Uwanja wa Olympia Park, Rustenburg Afrika Kusini kuvaana na Swaziland katika michuano ya Baraza la Vyama vya Soka Kusini mwa Afrika (Cosafa).

Tanzania itashuka uwanjani katika mechi hiyo ya Kundi B, itakayopigwa majira ya saa 2:00 usiku kwa saa za Afrika Mashariki ikiwa kama nchi alikwa kwenye michuano hiyo.

Kocha Mkuu wa timu ya Taifa Stars, Mart Nooij, amesema kuwa wachezaji wake wako tayari kwa mchezo huo baada ya kufanya mazoezi kwa siku zote walizokuwa huko licha ya hali ya hewa ya kuwa ya baridi kali.


Nooij alisema wachezaji wake walitarajiwa kufanya mazoezi ya mwisho jana jioni kwa lengo la kujiandaa kuikabili Swaziland na kwamba wote wapo fiti.

"Hakuna mchezaji ambaye ameshindwa kufanya mazoezi licha ya hali ya hewa ya baridi, kila mmoja anajituma, ni dalili njema ndani ya timu kwa sababu tunahitaji kupata matokeo mazuri," alisema Kocha huyo.

Taifa Stars ambayo ni timu alikwa kwenye michuano hiyo inayofanyika kila mwaka itashuka tena Jumatano Mei 20 mwaka huu kuivaa Madagascar na itamaliza mechi zake za hatua ya makundi Ijumaa kwa kucheza na Lesotho.

Mshindi wa kila kundi ataungana na wenyeji Afrika Kusini, Msumbiji, Zambia, Ghana, Botswana na Malawi kucheza hatua ya robo fainali.

Kutakuwa na nusu fainali za aina mbili, kwanza za timu zilizofungwa katika robo fainali na zilizoshinda kwenye hatua hiyo.

Pia timu vibonde zitaendelea kupepetana hadi fainali yao ambayo itapigwa Mei 29, wakati fainali ya wakali itakuwa Mei 30.

Baada ya kumaliza mashindano hayo, Taifa Stars itaendelea na mazoezi kwa ajili ya mechi zake mbili zinazofuata dhidi ya Misri (mechi za mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika- Afcon) na baadaye Uganda kwenye michuano ya kuwania tiketi ya kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN).

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC