Ruka hadi kwenye maudhui makuu

WADAU WAMPONDA KOCHA STARS, WADAI BORA YA KIM POULSEN

Wachambuzi wa soka wamesema timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ haina kiwango cha kuvutia uwanjani na imepoteza mvuto.

Wakizungumza baada ya kuishuhudia Taifa Stars ikilazimishwa sare ya bao 1-1 na Malawi katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa uliofanyika Mwanza juzi, walisema wanauona mwisho mbaya wa kocha Mholanzi, Mart Nooij.

Kocha Joseph Kanakamfumu aliliambia gazeti hili kuwa Nooij hajaibadilisha Stars na inacheza ili mradi tu tofauti na mtangulizi wake, Kim Poulsen.

Kanakamfumu alisema jambo kubwa analokosea Mholanzi huyo ni uteuzi wa kikosi chake, hasa aina ya wachezaji anaowaita kwani wengi wao hawako fiti.


“Nikiangalia hajaibadilisha timu tofauti na wakati wa Kim kwani timu ilikuwa unaona kabisa inacheza mpira mzuri, lakini kwa huyu timu haichezi kwa mpangilio, hatuoni mtiririko mzuri uwanjani, kila mchezaji anajichezea anavyojua yeye,” alisema Kanakamfumu.

Aliongeza: “Tatizo kubwa anapokosea ni kwenye uteuzi wa timu yake, inatakiwa aangalie wachezaji anaowaita wapo vizuri namna gani kulingana na mfumo anaoutumia, kwani wachezaji wengi aliowaita hawaendani na mfumo wake wa kujilinda.”

Naye Eugine Mwasamaki alisema tatizo liko kwa kocha na hata wachezaji wake kwani kiwango cha timu hiyo si kizuri na kinasikitisha.

Mwasamaki alisema anachoshangaa ni Nooij kuwaita kikosini wachezaji ambao hata kwenye klabu zao hawachezi na kuwacha wengi wanaoonyesha viwango vizuri kwenye mechi Ligi Kuu Bara.

Wachezaji ambao hawana namba ya kudumu katika klabu zao kwa sasa, lakini wapo Stars ni pamoja na Mwadin Ally, Amri Kiemba, Deo Munishi na John Bocco.

“Nashangaa, inawezekana kocha mwenyewe ana matatizo au wanaomsaidia hawana sifa za kumsaidia, kwani kadri muda unavyokwenda kiwango cha timu kinaporomoka. Niseme tangu kuondoka kwa Maximo kwenye timu ya Taifa, hakuna kocha mwingine aliyeleta mabadiliko ndani ya timu hii,” alisema Mwasamaki.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...