Ruka hadi kwenye maudhui makuu

PLUIJM AKIRI YANGA KUBANWA NA STAND UTD

Licha ya timu yake kuibuka na ushindi wa mabao 3-2 juzi, kocha wa Yanga, Hans van der Pluijm, amesema kuwa wapinzani wao Stand United kutoka Shinyanga waliwazidi uwezo katika mchezo huo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Wageni Stand ndiyo walikuwa wa kwanza kuliona lao la Yanga lakini baadaye wenyeji walisawazisha na kuongeza la pili lililodumu hadi mapumziko. Stand walisawazisha mapema kipindi cha pili, kabla ya Yanga kupata penalti iliyowapa ushindi wa 3-2 katika dakika za lalasalama.

Akizungumza juzi baada ya mechi hiyo, Pluijm alisema kwamba kikosi chake hakikucheza vizuri, wachezaji hawakuwa na maelewano katika mchezo huo licha ya kushinda.


Alisema kuwa pengo la mabeki, Nadir Haroub 'Cannavaro' na Kelvin Yondani, lilionekana wazi katika mechi hiyo ambayo Stand United ilionyesha soka la kiwango cha juu licha ya kuwa ugenini.

"Timu ilifanya makosa kadhaa, kulikuwa hakuna mawasiliano kati ya Twite (Mbuyu) na Rajab (Zahir), hawakuweza kuzuia mashambulizi ya mara kwa mara yaliyokuwa yanakuja kwenye lango letu, kwa kifupi hatukucheza vizuri," alisema Pluijm, raia wa Uholanzi.

Aliongeza kwamba amepona mapungufu hayo na kuahidi kuyafanyia kazi na kuwaweka wachezaji wote kuwa tayari kuziba mapengo ya wenzao pale watakapohitajika.

Naye kocha wa Stand United Mganda, Martin Lule, alisema kwamba timu yake imepoteza mchezo huo kwa bahati mbaya lakini vijana wake walionyesha soka la kuvutia.

Mganda huyo alisema kwamba Yanga ni timu ya kawaida na kiwango chake si cha kuhofia hivyo anaahidi msimu ujao atahakikisha hapotezi tena dhidi ya vinara hao wa ligi kuu.

"Yanga inawachezaji wa kawaida, tumefungwa kama mechi nyingine tunavyofungwa, haina wachezaji tofauti na timu nyingine, wana viwango vya kawaida," aliongeza kocha huyo.

Baada ya ushindi huo wa juzi, Yanga ilifikisha pointi 49 na hivyo kuhitaji pointi sita tu ili kutangazwa mabingwa wapya wa ligi wakati Stand United yenye pointi 28 iko katika nafasi ya nane kwenye msimamo.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC