Ruka hadi kwenye maudhui makuu

HATA KAMA KUNA MACHAFUKO, NAKWENDA TU SAUZI- NGASSA

Winga wa Yanga ya jijini Dar es Salaam, Mrisho Ngasa, amesema kwamba licha ya hali ya machafuko inayoendelea nchini Afrika Kusini ya wazawa dhidi ya wageni, hatasita kwenda huko endapo atapokea mwaliko wa kujiunga na klabu yoyote  itakayomuhitaji.

Ngasa ambaye alirejea Yanga akitokea Simba kwa mkopo, anatarajia kumaliza mkataba wake Jangwani mwezi ujao.

Ngasa ambaye mwaka jana alikwenda Afrika Kusini kufanya majaribio 'kinyemela', anatajwa kuwa kwenye mipango ya kuhamia Free State Stars ya huko na ndio inayofanya achelewe kusaini mkataba mpya na Yanga.


Akizungumza jana jijini, Ngasa alisema kwamba yeye ni mchezaji na yuko tayari kwenda Afrika Kusini kujiunga na timu yoyote itakayoridhishwa na kiwango chake.

Mshambuliaji huyo ambaye juzi alifunga goli moja katika ushindi wa 3-2 dhidi ya Stand United, alisema kwamba soka ndio ajira yake hivyo anaamini kwamba akipata nafasi ya kwenda Afrika Kusini au nchi nyingine atakwenda kucheza mpira sehemu iliyo salama kwa sababu hatakuwa peke yake uwanjani.

"Mimi ni mwanajeshi, nitakwenda vitani wala sitaiachia fursa hiyo ikitokea, kiukweli wala sitahofia," alisema mshambuliaji huyo.

Alisema kwamba bado anaamini ana nafasi ya kwenda kucheza soka nje ya nchi na pia kuitumikia timu ya taifa (Taifa Stars) kwa muda mrefu.

Nyota huyo sasa amekuwa na ndoto za kucheza soka la kulipwa tofauti na mwaka 2012 alipokataa ofa ya kujiunga na El Merreikh ya Sudan iliyomuhitaji wakati huo akiwa anaichezea Azam.

Kutokana na Ngasa kukataa ofa ya El Merreikh na kuonyesha mapenzi yake kwa Yanga kwa kuibusu nembo ya klabu hiyo, Azam ilimtoa kwa mkopo Simba ambako aliitumikia kwa msimu mmoja.

Mbali na Ngasa, mchezaji mwingine wa Yanga aliye katika kikosi cha kwanza ambaye anamaliza mkataba mwezi ujao ni Mnyarwanda Haruna Niyonzima.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC