Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SIMBA KUVAANA NA TAIFA JANG'OMBE ILIYOSHINDA KWA SHILINGI

Wapinzani wa Simba katika hatua ya robo-fainali ya michuano ya Kombe la Mapinduzi visiwani hapa wamepatikana kwa kurusha shilingi baada ya timu mbili za Kundi A, Polisi na Taifa ya Jang'ombe kumaliza katika nafasi moja.

Polisi, wawakilishi wa Zanzibar katika michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika mwaka huu, na Taifa ya Jang'ombe jana walimaliza mechi zao za hatua ya makundi wakitoka suluhu kwenye Uwanja wa Mao Tse Tung visiwani hapa.

Matokeo hayo yaliwafanya wote wamalize nafasi ya pili katika msimamo wa Kundi A linaloongozwa na Yanga wakiwa wamefanana kwa kila kitu baada ya wote kufungwa 4-0 dhidi ya Yanga kisha wote kuifunga Shaba FC ya Pemba bao 1-0.


Baada ya kumalizika kwa mechi kati ya timu hizo jana, Chama cha Soka Zanzibar (ZFA) na Kamati ya Mashindano hayo walikutana na kuamua kurusha sarafu kwenye Uwanja wa Amaan kabla ya mechi ya Yanga dhidi ya Shaba FC saa mbili usiku jana.

Kinara wa Kundi C, Simba anakutana na 'best looser 2', (Polisi/Taifa) kwenye Uwanja wa Amaan leo.

GORAN AIPONDA SIMBA
Baada ya kuvuka kiunzi kwa JKU, Simba imefanikiwa kukwepa kukutana na timu ngumu za Azam FC na KCCA FC ya Uganda katika hatua ya robo-fainali ya michuano hiyo itakayochezwa kwenye Uwanja wa Amaan visiwani hapa leo.

Kikiwa na kocha mkuu mpya, Goran Kopunovic, kikosi cha wekundu hao wa Msimbazi kiliibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya JKU katika mechi kali ya mwisho ya Kundi C iliyopigwa kwenye Uwanja wa Amaan, mechi iliyompa ushindi wa pili mfululizo Mserbia huyo katika mechi mbili alizoiongoza timu hiyo tangu asaini mkataba wa miezi sita siku ya mwaka mpya.

Ushindi huo pia umeifanya Simba imalize kileleni mwa msimamo wa Kundi C ikiwa na pointi sita, moja juu ya Mtibwa Sugar walioko nafasi ya pili, hivyo kukwepa kukutana na timu ngumu za Kundi B, KCCA na Azam FC katika hatua inayoanza leo ya robo-fainali.

Goli lililoipeleka Simba fainali lilifungwa na winga Ramadhan Singano 'Messi' dakika nne kabla ya robo saa ya mchezo akiitendea haki kwa kupiga shuti kali la mguu wa kushoto pasi ya 'kuchopu' ya kiungo Said Ndemla baada ya kazi nzuri ya mshambuliaji Mganda Sserunkuma aliyepiga chenga nyingi mabeki wa kikosi cha kocha Malale Hamsini cha JKU.

Mara tu baada ya mechi hiyo, Goran aliiponda Simba iliyoanza na wachezaji wawili wa kigeni, Waganda Juuko Murushid na Dan Sserunkuma akidai bado ina tatizo la kukata pumzi.

Kocha huyo alisema: "Tunamshukuru Mungu kwa ushindi huu wa pili lakini timu yangu bado ina udhaifu mkubwa. Bado tuna tatizo la kukosa pumzi, wachezaji wanaonekana hawako fiti."

"Tumecheza vizuri hadi dakika ya 27 na baada ya hapo tukaonekana kuzidiwa na wapinzani wetu kutokana na pumzi yetu kuonekana ndogo. Ninajua chanzo cha tatizo hili, nitalitatua kwa mbinu ambazo siwezi kuziweka wazi kwa sasa," alisema zaidi Mserbia huyo.

Kundi C:        P  W   L   D  GF  GA GD  PTS
1. Simba        3   2   1    0    2     1     1     6
2. Mtibwa     3   1   0    2    2     1     1     5  
3. JKU         3   1   1    1    3     2     1     4
4. Mafunzo   3   0   2    1   O    3    -3     1


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...