Ruka hadi kwenye maudhui makuu

PLUIJM APONDA MASTRAIKA WACHOYO YANGA

Kocha wa Yanga, Hans van der Pluijm amewajia juu washambuliaji wa timu hiyo kutokana na kukosa magoli mengi na amewataka kuacha uchoyo baina yao kwa manufaa ya timu.

Licha ya kushinda kwa idadi kubwa ya mabao (4-0) katika mechi zao mbili za kwanza za Kombe la Mapinduzi, wachezaji wa Yanga walikuwa wakikosa magoli mengi ambayo yangeweza kuwafanya kupata ushindi mnono zaidi.

Yanga ilitolewa katika robo fainali ya mashindano hayo maalum ya kuadhimisha Mapinduzi ya Zanzibar kwa goli 1-0 la dakika za lalasalama la JKU ya Zanzibar huku miamba hao wa soka wa Tanzania Bara wakiwa tayari wamekosa magoli mengi kupitia kwa washambuliaji wao Amisi Tambwe na Kpah Sherman.


Akizungumza jana katika makao makuu ya klabu hiyo Jangwani jijini Dar es Salaam kabla ya kwenda Bagamoyo kuweka kambi ya kujiandaa na mechi yao ua Ligi Kuu ya Bara dhidi ya Ruvu Shooting, kocha huyo Mholanzi alisema amebaini kuna tatizo la ushirikiano katika umaliziaji na aliwataka washambuliaji kushirikiana zaidi ya sasa.

Alisema amewaelezea wachezaji wake kwamba ni lazima washirikiane kwa sababu mafanikio ama kushindwa kunakuwa ni kwa timu nzima na si mchezaji mmoja mmoja, hivyo waweke mbele kusaka mafanikio ya pamoja.

Pluijm alisema walipoteza nafasi nyingi za kufunga katika mechi zao za Kombe la Mapinduzi na kwamba hatapenda kuona mapungufu hayo yanajirudia katika Ligi Kuu ya Bara.

"Tunajitahidi kurekebisha makosa madogo yaliyojitokeza katika Kombe la Mapinduzi ili iwe tofauti tutakaporejea kwenye Ligi  Kuu," alisema Pluijm.

Akizungumzia maandalizi ya mechi yao ya Jumamosi dhidi ya Ruvu Shooting, alisema timu hiyo ya mkoani Pwani siyo ya kubeza licha ya kwamba msimu uliopita waliifunga 7-0 katika mechi ya ligi kuu.

"Hakuna mechi nyepesi msimu huu, utaona timu kubwa inafungwa dhidi ya timu ndogo, kinachotakiwa ni maandalizi na kupanga kikosi imara," alisema Mholanzi huyo aliyerejeshwa kuchukua nafasi ya Mbrazil Marcio Maximo aliyetimuliwa baada ya mechi saba tu za mzunguko wa kwanza.

Alisema kikosi chake kimebadilika tangu aanze kukifundisha na kwamba anachofanya ni kuendelea kufanyia kazi mapungufu machache ili kiwe tishio kwenye ligi.

Alisema atahakikisha timu yake haipotezi mechi kuanzia mchezo wao ujao Jumamosi dhidi ya Ruvu Shooting na mechi inayofuata dhidi ya Coastal Union Jumatano ijayo ugenini Tanga.

Yanga inashika nafasi ya pili katika msimamo ikiwa na pointi 14, mbili nyuma ya vinara Mtibwa Sugar.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC