Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KOPUNOVIC AAHIDI KUTINGA FAINALI LEO NA POLISI ZANZIBAR

Kocha Mkuu wa Simba, Goran Kopunovic amesema kikosi chake kimeimarika na kinampa matumaini ya kushinda mechi yao ya leo ya nusu-fainali ya Kombe la Mapinduzi dhidi ya Polisi na kutinga fainali ya michuano hiyo.

Mechi hiyo itatanguliwa na mechi ya nusu-fainali ya kwanza ya Mtibwa Sugar dhidi ya wababe wa Yanga, timu ya JKU, mechi zote zikichezwa kwenye Uwanja wa Amaan visiwani hapa saa 10:00 jioni na saa 2:15 usiku.

Goran alisema visiwani hapa jana kuwa: “Kikosi chetu kinazidi kuimarika, jana (juzi) tulianza mazoezi maalum kwa ajili ya mechi ya nusu-fainali na ninaona tuko katika hali nzuri."

"Kuna vijana wazuri nimewakuta kikosini, ninaamini tutafanya vizuri na kusonga mbele,:" alisema zaidi Mserbia huyo.

Simba ilifanikiwa kutinga nusu-fainali ikiiadhibu kwa kipigo hicho kikali timu ya Daraja la Pili visiwani hapa Taifa ya Jang'ombe katika mechi yao ya robo-fainali Jumatano, shukrani kwa mabao ya kiungo mshambuliaji Ibrahim Hajibu aliyepiga 'hat-trick' dakika za 46, 62 na 75 kabla ya kiungo mshambuliaji Shaba Kisiga kufunga la nne dakika 10 kabla ya nusu sasa ya tatu ya mchezo.


Hata hivyo, katika mahojiano na gazeti hili visiwani hapa jana mchana, Kocha Mkuu wa Polisi, Hamis Sufian alisema: "Nimekuwa nikitumia muda mwingi kuangalia mechi za Kombe la Mapinduzi. Nilifanikiwa kuisoma vizuri KCCA. Wembe uliotumika kuinyoa, ndiyo ule ule utakaotumika kuinyoa Simba maana nao pia nimewasoma."

Polisi imetinga nusu-fainali baada ya kuwavua ubingwa kwa matuta KCCA ya Uganda katika mechi kali ya robo-fainali iliyomalizika kwa suluhu katika dakika 90 za kawaida.

MTIBWA vs JKU NI VITA

Katika hatua nyingine, Kocha Mkuu wa Mtibwa Sugar, Mecky Mexime amesema anazitambua vyema mbinu za Kocha Mkuu wa JKU, Malale Hamsini ambaye leo timu zao zinapambana katika mechi ya kwanza ya nusu-fainali.

"JKU ni timu nzuri na ngumu, ina mfungaji mzuri (Amour Omary) Janja ambaye nimemuona hapa anafunga mabao mazuri. Goli lake la jana ninafikiri ni bao bora la mashindano haya mwaka huu.

"Kocha Mkuu wa JKU ni 'classmate' (mwanafunzi mwenzake) wangu katika ukicha. Ninazifahamu mbinu zake na yeye anazijua za kwangu. Mashabiki waje waone kitakachotokea maana na sisi tuna kikosi kizuri msimu huu," alisema Mexime katika mahojiano maalum na gazeti hili visiwani hapa jana mchana.

Baada ya kuing'oa Yanga juzi, Malale alisema atajipanga vizuri kuhakikisha anakuwa kocha wa kwanza kuifunga Mtibwa katika mechi za mashindano msimu huu.

Mtibwa na JKU zilikutana katika mechi ya mwisho ya Kundi B iliyomalizika kwa sare ya bao moja, mabao yakifungwa na Mussa Hassan 'Mgosi'dakika ya 20 na baadaye alikosa penalti kabla ya 'mbaya wa Yanga', Janja kuisawazishia timu yake dakika ya 72.

Safu ya ulinzi ya Mtibwa Sugar inayoongozwa na mchezaji bora wa mechi iliyopita ya robo-fainali dhidi ya Azam FC, Salim Mbonde, inapaswa kumchunga kwa uangalifu mkubwa Janja kwani mfungaji huyo bora wa Ligi Kuu ya Zanzibar msimu uliopita na kinara wa mabao kwa sasa katika ligi hiyo(mabao nane) ana miguu inayolijua goli lilipo.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...