Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KASEJA AWAAMBIA YANGA MSINITANIE MIMI BADO JANGWANI.

Mlinda mlango Juma Kaseja ameshtushwa na habari za kutimuliwa kwake na Yanga na kudai yeye hatambui maamuzi hayo kwani yametolewa nje ya muda muafaka wa usajili pili hajapewa barua ya kufukuzwa kwake.

Kaseja amesema yeye bado mchezaji halali wa Yanga na hatambui suala la kutimuliwa kwake.

Juzi uongozi wa Yanga ulitangaza kuachana na mlinda mlango Juma Kaseja kwa madai hajaripoti kwenye kituo chake cha kazi kwa muda mrefu na hajulikani halipo.


Kupitia kwa mkuu wa idara ya habari na mawasiliano wa Yanga Jerry Muro amesema Yanga imeamua kuachana na Kaseja kwakuwa alikuwa mzigo kwao.

Kaseja aliingia matatizoni na klabu yake akiidai fedha zake za usajili zilizosalia ambazo ni mil 20, lakini uongozi wa Yanga ulimalizana naye kwa kumwekea ktk akaunti yake fedha hizo.

Kaseja aliendelea kulumbana na Yanga safari hiyo akilalamikia kitendo cha kuwekwa benchi na kudai wamekiuka mkataba waliokubaliana ambao ulikuwa unasema atakuwa kipa wa kwanza.

Lakini uongozi wa Yanga umekiuka masharti ya mkataba na kumwambia mwenye suala ya kuamua nani awe kipa wa kwanza ni mwalimu kitendo kilichopelekea yeye kusugua benchi karibu mechi zote ilizocheza Yanga zikiwemo za kirafiki.

Juzi uongozi wa Yanga ulitangaza kuachana naye na kuna mipango ya kutaka kumfungulia kesi ya kudai fidia kwa madai kuwa Kaseja amevunja mkataba kwa kutoweka kwenye eneo lake la kazi jambo ambalo Kaseja anapinga na kusema yeye anatambua ni mchezaji halali wa Yanga na walka hajapewa barua ya kuachwa na akipewa atazungumza na waandishi wa habari

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...