Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Equatorial Guinea walenga Kombe la Dunia

Esteban Becker

Kocha mwenye ndoto kubwa wa wenyeji wa Kombe la Mataifa ya Afrika, Equatorial Guinea, Esteban Becker amehimiza vijana wake watumie dimba hilo kama ngazi ya kufuzu Kombe la Dunia.

Becker wa kutoka Argentina ambaye alichukua utawala wa Nzalang Nacional mapema mwezi huu, amekuwa na majuma mawili pekee kuandaa kikosi chake kujitosa uwanjani nyumbani wakati shindano hilo litakapongoa nanga Jumamosi dhidi ya Congo Brazzaville jijini Bata kwenye Kundi A.

Ingawa kufuzu robo fainali ya awamu ya 2012 wakati nchi hiyo iliandaa kwa pamoja na Gabon ni lengo mufti, Becker anatizama mbele zaidi na azima yake ya kuwaongoza kuingia Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza kwenye historia yao.

“Naota kila wakati kushiriki Kombe la Dunia kwa hivyo bidii zangu zote zitaelekezwa kutayarisha kikosi chetu changa kuwa na nafasi ya kuwania tiketi ya kucheza dimba hilo lijalo la 2018,” Becker ambaye aliongoza kikosi cha taifa cha wanadada cha taifa hilo kinyakua ubingwa wa Afrika miaka mitatu iliyopita aliongeza.


Equatorial Guinea wanashiriki dimba la Mataifa kufuatia kujiondoa kwa Morocco kama wenyeji Novemba iliyopita na utawala wa taifa hilo ndogo kukubali mwito wa shirikisho la kandanda la Afrika CAF kuchukua mahala pao kama wenyeji wa dharura.

“Tuna wachezaji wenye uzoefu (Javier) Balboa na Juvenal (Edjogo-Owono) na chipukizi ambao wanachezea vilabu vizuri Uhispania kama Mallora, Malaga na Valencia.
“Tumekusanya pamoja kundi la wachezaji wenye ari kwa siku kumi pekee, kimawazo, wana nguvu za kustahimili na wameimarika na mbinu,” aliongeza.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC