Ruka hadi kwenye maudhui makuu

REAL MADRID YAENDELEZA REKODI YAKE YA USHINDI

Karim Benzema

Cristiano Ronaldo alifunga mawili na kusaidia viongozi wa La Liga Real Madrid kutwanga Almeria 4-1 na kuongeza mkimbio wao wa kushinda hadi mechi 20 Ijumaa.

Ronaldo alifunga dakika 10 za mwisho na kufikisha idadi ya mabao aliyofunga ligini hadi 25 alipofikia mpira wa Karim Benzema uliokuwa umezimwa na kisha akafunga kutoka kwa pasi ya Isco kutoka katikati ya eneo la hatari na kukamilisha ushindi huo.

Real wanaongoza jedwali la ligi na alama 39 kutoka kwa mechi 15, alama tano mbele ya Barcelona watakaotembelea Getafe Jumamosi.

Kiungo wa kati Isco alikuwa ameweka Real kifua mbele kwa kombora kali la kujipinda kutoka nje ya eneo la hatari dakika ya 15 kabla ya Almeria kusawazisha kwa kombora la mbali lililotoka kwa Verza.

Gareth Bale kisha alifunga kwa kichwa kutokana na krosi ya Toni Kroos na kuweka Real 2-1 mbele wakati wa mapumziko.


Kipa Iker Casillas baadaye aliweka wageni mbele kwa kukomboa penalti ya Verza katikati ya kipindi cha pili kabla ya Ronaldo kufunga mabao yake mawili.

Real watasafiri Morocco wiki ijayo kwa Kombe la Dunia la Klabu wakiwa na mechi mbili zaidi walizoshinda ikilinganishwa na mkimbio bora zaidi wa awali wa klabu ya Uhispania uliowekwa na Barcelona wa mechi 18 kuanzia Oktoba 2005 hadi Januari 2006.

Almeria, waliomfuta kocha wao Francisco Rodriguez Jumanne iliyopita na wakammteua Juan Ignacio Martinez kuwa mrithi wake kufuatia mechi hiyo ya Real, wamo eneo la kushushwa ngazi wakiwa na alama 10.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC