Ruka hadi kwenye maudhui makuu

RA,OS AMALIZA MWAKA BORA KWA TUZO YA CWC

Sergio Ramos

Difenda wa Real Madrid aliyeshinda mataji mengi Sergio Ramos ametaja mwaka 2014 "mwaka bora zaidi maishani mwangu” baada ya kuchangia sana ufanisi wa miamba hao wa Uhispania waliposhinda mataji manne ikiwa ni pamoja na kutwaa kombe la Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya mara ya 10.

Mkabaji huyo wa kati ambaye nguvu zake angani mara nyingi huzalisha mabao alishinda tuzo ya mchezaji wa dimba katika Kombe la Dunia la Klabu baada ya kufunga wakati wa ushindi nusufainali dhidi ya Cruz Azul na ushindi dhidi ya San Lorenzo kwenye fainali Jumamosi.
Tukio kuu zaidi uwanjani katika mwaka ambao pia alikuwa baba kwa mara ya kwanza lilikuwa kusawazisha dakiak za mwisho dhidi ya Atletico Madrid fainali ya Kombe la Klabu Bingwa Ulaya Mei kabla ya Real kushinda mahasimu hao wao wa jiji 4-1 baada ya muda wa ziada kuongezwa.


Mabao yake dhidi ya Cruz Azul, San Lorenzo na Atletico yalikuwa ya kawaida ya ufungaji kwa kichwa michezo ya kupangwa na ilitia nguvu zaidi nafasi ya mzaliwa huyo wa Seville mwenye miaka 28 kama shujaa miongoni mwa mashabiki wa Real.

Ramos mwenye chale nyingi pia alikuwa mchezaji muhimu kwenye timu ya Uhispania iliyoshinda mfululizo mataji ya Ubingwa Ulaya 2008 na 2012 na Kombe la Dunia mara ya kwanza hapo katikati.
Kushindwa kwa Uhispania kutetea taji la Kombe la Dunia Brazil mwezi Juni kuliwa doa kuu lakini Ramos hata hivyo alitangaza mwaka 2014 kama “muhimu zaidi maishani mwangu, uwanjani na maisha yangu binafsi.”

"Nilikuwa na tukio kuu la kuwa baba na kwenye uchezaji niliweza kushinda mataji manne na kombe la Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya ambalo tulitaka sana,” aliambia kituo cha redio cha Cadena Ser baadaye Jumapili.
“Kushinda tuzo hufurahisha sana lakini ni kupitia bidii ya wachezaji wenzangu na ikiwa mchezaji binafsi anang’aa ni kutokana na juhudi zao.”

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...