Ruka hadi kwenye maudhui makuu

PHIRI ASEMASIMBA SASA IMEIVA, ANAYEKATIZA MBELE HALALI YAO

Baada ya kuichapa Yanga mabao 2-0 na kufanikiwa kunasa saini za nyota watatu wapya kutoka Uganda, kocha wa Simba, Mzambia Patrick Phiri alisema kikosi chake sasa kimeiva na anaamini kitafanya kazi nzuri msimu huu.

Simba iliinyanyasa bila huruma Yanga kwa kuipa kipigo cha pili katika mechi ya Nani Mtani Jembe 2 iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Jumamosi.

Katika mechi hiyo, Simba iliwatumia wachezaji wawili kutoka Uganda waliokuwa wametua nchini kwa ajili ya kufanya majaribio, beki Juuko Murshid na mshambuliaji Simon Sserunkuma kabla ya juzi kuwasanisha mikataba baada ya kuridhika na viwango vyao.

Katika mahojiano na NIPASHE jijini jana, Phiri alisema kikosi chake kimeimarika na kinampa matumaini ya kufanya vizuri katika mechi zinazofuata za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) msimu baada ya kuanza vibaya katika mechi sita za awali walizoambulia sare.

"Kesho (leo) tutaanika wachezaji wote walioingia na kutoka Simba kabla ya timu yetu kuingia kambini Ndege Beach (Dar es Salaam) mwishoni mwa wiki kujiandaa kwa VPL.


"Nisingependa kuongelea kuachwa kwa (Amissi) Tambwe na (Pierre) Kwizera kwa sababu muda wa usajili haujafungwa na suala hilo litaelezwa na uongozi kesho (leo).

"Kikubwa nilikuwa ninasaka muunganiko mzuri wa timu ambao sasa umeanza kuoneakana. Tumekuwa na mwanzo mbaya katika ligi ndiyo maana tumelazimika kufumua kikosi kwa kiasi kikubwa," alisema Phiri.

UHURU AVUNJA MKATABA

Katika hatua nyingine, kiungo mshambuliaji wa klabu ya hiyo Uhuru Seleman ameweka wazi kuwa ombi lake kuitaka Simba ivunje mkataba wake limekubaliwa.

"Nilituma barua ya kuomba klabu isitishe mkataba wangu bila malipo ili niweze kuwa huru kutafuta timu nyingine ya kuchezea, ninashukuru sana uongozi wa Simba umelikubali ombi langu. Sasa nipo huru," alisema Uhuru jijini jana.

Alisema anatarajia kujiunga na Mwadui FC ya mkoani Shinyanga inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara (FDL) ili kuboresha kiwango chake kabla ya kwenda Afrika Kusini kufanya majaribio ya kujiunga na Klabu ya Jomo Cosmos.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC