Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MOURINHO AFURAHISHWA SANA NA VIJANA WAKE

Jose Mourinho

Meneja wa Chelsea Jose Mourinho alisifu sana ushindi wa vijana wake wa 2-0 Ligi ya Premia ugenini Stoke City Jumatatu na kuutaja kuwa mojawapo ya ushindi muhimu zaidi wao msimu huu.

Bao la kichwa dakika ya pili kutoka kwa John Terry na la Cesc Fabregas kipindi cha pili, yaliwezesha vijana hao wa London kurejesha mwanya wa alama tatu kileleni mwa jedwali kati yao na Manchester City klabu zikielekea Krismasi.

Lakini ni jinsi ushindi huo ulivyopatikana iliyomfurahisha Mourinho sana huku Chelsea wakipigana kushinda vita vikali vya kimwili.
“Kushinda hapa lazima ucheze mchezo mzuri sana na tulifanya hivyo kwa sababu tulibadilika na mtindo wao wa uchezaji,” akasema.

“Tulipokuwa na mpira, tulijaribu kutopoteza sifa zetu na kucheza mchezo wetu.
“Huwa wakali sana uwanja huu, na mashabiki huwaunga mkono sana. Wana wachezaji wazuri na benchi zuri pia. Ulikuwa ushindi mgumu.


“Ni ushindi ambao una maana zaidi ya alama tatu. Haikuwa tu vigumu lakini unahitaji zaidi ya ustadi wako pekee kushinda hapa.

“Wachezaji walikabiliana vyema na mtindo huo mgumu na hawakuogopa kuwajibika na wachezaji wetu wabunifu hawakuogopa kukabili mechi.

"Wachezaji wetu wa kujilinda walikuwa ngangari sana. Ni kwa kuwa na uchezaji mzuri sana wa timu ambapo iliwezekana kushinda Stoke.”

Mourinho pia alimsifu nahodha wake Terry aliyefunga katika Ligi ya Premia kwa msimu wa 15 mfululizo.
“Huwa hatari sana michezo ya kupangwa, ni mchezaji mzuri sana angani, daima huwa hatari,” akasema.
“Muhimu zaidi ni jinsi amekuwa akicheza msimu huu tena. Nilipofika hapa mwaka jana alikuwa katika matatizo kiasi, uchezaji wake ulikuwa na panda shuka. Hakuwa akichezea Chelsea sana.
"Lakini ghafla miaka miwili iliyopita, anacheza karibu kila mechi na kwangu katika kiwango sawa ana alichokuwa nilipokuwa hapa 2004-2007.

"Ni kutokana na njia yetu ya kufanya kazi. Aliingiliana vyema sana na njia yetu ya mazoezi na mwili wake.
"Anajihisi mkali na mwenye kasi katika hali nzuri, Ana furaha na unapokuwa na furaha na unajiamini basi huwa rahisi katika kila kazi. Kandanda huhitaji sana hili. Anajua namwamini na ana imani na anacheza vyema sana.”

Mkabaji kamili wa Stoke Phil Bardsley alionyeshwa kadi ya njano pekee kwa kumpiga ngwara nyota wa Ubelgiji Eden Hazard kipindi cha kwanza lakini Mourinho, aliyechemka sana wakati huo, alifikiri alifaa kufukuzwa uwanjani.

“Kwa maoni yangu na mwilini, inaonekana kama ilikuwa kadi nyekundu lakini sijui,” akasema Mourinho.
"Nijuacho ni kwamba ikiwa alicheza visivyo, kilikuwa kisa pekee. Ilikuwa mechi safi lakini ya kukaripiana sana. Refa alidhibiti mechi. Wachezaji walicheza haki.

“Vilikuwa vita vyema. Nguvu za mwili, kukabiliana moja kwa moja, mipira mingi ya mbali. Lakini mechi ilikuwa safi kabisa na sahihi. Iwapo ilikuwa kadi nyekundu kilikuwa kisa pekee. Na tunahitaji kutilia maanani hilo.”

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC