Ruka hadi kwenye maudhui makuu

JONAS MKUDE MBIONI KUTUA YANGA, AZAM NAYO YAMTAKA NDEMLA

SIMBA huenda wakapata pigo kubwa kama hawatafanya jitihada za kukaa chini na wachezaji wao muhimu ambao mikataba yao iko ukingoni.

Miongoni mwa wachezaji hao ni Jonas Mkude na Said Ndemla ambao kwa sasa wanaruhusiwa kufanya mazungumzo ya awali na klabu yoyote.

Gazeti hili linajua kuwa Simba walianza mikakati jana Jumapili ya kuweka mambo sawa lakini wapinzani wao Yanga na Azam wameshashtukia dili na ndio wanafanya mikakati ya chinichini kuwanasa wachezaji hao muhimu kwa Simba.

Habari za uhakika kutoka Yanga ambazo gazeti hili inazo ni kwamba wameelekeza nguvu zao kwa Mkude huku wakisisitiza kwamba ndiye mchezaji pekee wa Simba kwa sasa mwenye hadhi ya kuichezesha na kusukuma mashambulizi kwenye mzunguko wa pili wa ligi na Kombe la Shirikisho ikielezwa kwamba hata mfumo wa Marcio Maximo unambeba.


Habari kutoka ndani ya uongozi wa Simba zinadai kwamba tofauti zilizopo kati ya wanachama wa kundi la Friends of Simba huenda zikaigharimu timu hiyo kwani baadhi yao wamekuwa wakivujisha siri za uongozi kwa wapinzani wao Yanga wanapokuwa vijiweni.

Mbaya zaidi imedaiwa kwamba baadhi yao ndio wanaowaondoa Ndemla na Mkude Simba kwani wameanza kutafuta mpaka timu na kuwasaidia wachezaji hao ushauri ili kuwakomoa viongozi wenzao kwa kile kinachodaiwa kwamba wamewaweka pembeni na hawataki kuyafanyia kazi mawazo yao kwenye mambo mbalimbali.

Azam yenyewe imedaiwa kwamba imemtengea Ndemla Sh40 milioni kwavile mkataba wake una miezi sita kama ilivyo kwa Mkude. Kwa mujibu wa kanuni za usajili mchezaji anaruhusiwa kufanya mazungumzo na klabu nyingine anapobakiza miezi sita, hivyo ni rahisi sasa kuanza mazungumzo na klabu yoyote ya Ligi Kuu Bara endapo wapo tayari kuondoka Simba.

Habari kutoka ndani ya Yanga ilisema kuwa wanasubiri ripoti ya kocha wao Mbrazil Marcio Maximo ambayo itatoka baada ya kumaliza mechi mbili zijazo dhidi ya Mgambo na Azam. Lakini Azam na Ndemla wameshaanza mazungumzo.

Dirisha dogo la usajili linatarajia kufunguliwa rasmi Novemba 15 na kufungwa Desemba 15 mwaka huu, hivyo kila timu kwa sasa inatafuta jinsi ya kupata wachezaji wazuri wa kuimarisha vikosi vyao.

Yanga ina tatizo la kiungo mkabaji na hivyo kulazimika kumtumia Mbuyu Twite ambaye anamudu zaidi kucheza nafasi ya beki wakati Azam kama watamsajili Ndemla basi atakabiliana na upinzani kutoka kwa Salum Aboubakar ‘Sure Boy’.

“Tunasubiri ripoti ya kocha Maximo, lakini tumejaribu kuangalia ni mchezaji gani anaweza kutufaa, kwa pale Simba ni Mkude pekee hakuna mwingine, safu yetu ya kiungo inatakiwa kuimarishwa ila hatuwezi kuamua wenyewe mpaka kocha ashirikishwe,” alisema kiongozi huyo wa Yanga.

Wakati Mkude na Ndemla wakibakiza muda mfupi kuichezea Simba imeelezwa kuwa wachezaji wengi waliosajiliwa kutoka U-20 akiwemo Ramadhan Singano ‘Messi’, Haroun Chanongo ni miongoni mwa wachezaji wanaomaliza mikataba yao.

Yanga na Azam zikiwa kwenye mpango wa kuibomoa zaidi Simba ambayo mwenendo wake kwenye ligi ni wa kusuasua, Simba wao wamesema watahakikisha wanafanya jitihada za kuwafunga wachezaji hao kwa kuwapa mikataba mipya ingawa imedaiwa kuwa mchezaji kama Chanongo wanaweza kuachana naye.

“Ni kweli wachezaji hao Ndemla na Mkude wapo ndani ya mikataba ya miezi sita lakini kuna wengine ambao walitoka U-20 (sio kipindi hiki cha Rais Evans Aveava) nao wanamaliza mikataba yao na hapo hapo baadhi yao hawajamaliziwa fedha yao ya usajili akiwemo huyo Ndemla,” alisema mmoja wa viongozi wa Simba.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC