Ruka hadi kwenye maudhui makuu

COSTAL UNION FC KUMBURUZA ALIYEKUWA MFADHILI WAO "BINSLUM" MAHAKAMANI

UONGOZI wa Klabu ya Coastal Union ya Tanga umesema utakwenda mahakamani kuishtaki Kampuni ya Binslum Tyre kutokana na kitendo cha kutengeneza tisheti za Coastal Union zenye nembo ya kampuni Sound na kuwapa bure mashabiki kuingiza nazo kwenye mechi mbalimbali za ligi kuu Tanzania bara wakiwa wamelipiwa na viingilo vya mchezo husika.

Hali hiyo ni kinyume na utaratibu kutokana na kuwa tayari kampuni hiyo ilishajitoka kufadhili timu hiyo na tayari klabu ya Coastal Union ilikwishapata mfadhili mwengine ambayo ni kiwanda cha Kutengeneza Unga Ngano mkoani Tanga cha Pembe Flours Mills.


Kauli hiyo imetolewa kwenye kikao cha Kamati ya Utendaji Kilichoketi mwishoni mwa wiki ambapo kilikuwa na agenda nne za msingi ambazo ni Suala la mshambuliaji wa Coastal Union Danny Lyanga,Utoaji slipi benki,Jezi za Sound,Tarehe ya Uchaguzi.

Kikao hicho kilihudhuriwa na viongozi wa mbalimbali akiwemo Mwenyekiti wa Klabu ya Coastal
Union,Steven Mguto,Katibu Mkuu Kassim El Siagi,Mjumbe wa Kamati ya Utendaji,Albert Peter Saimu Amiri na Meneja wa Coastal Union Akida Machai.

Kimsingi suala ambalo lilikuwa gumzo ni suala la kampuni hiyo kuchukua hatua ya kuwavalisha mahsbiki wa Coastal Union jezi pamoja na kuwalipia viingilio vya mechi kwenye mechi mbalimbali za ligi kuu.

Kama unavyojua kuwa Kampuni ya Binslum Tyres ilikuwa mhisani wetu na sasa hatuko naye na tayari alishapeleka fedha zake kwenye vilabu vingine ikiwemo Mbeya City sasa tunamshangaa kuendelea kufanya biashara ya matangazo kupitia mashabiki wetu kwa kuwapa tisheti za kuvaa bure ikiwemo kuwalipia viingilio kwenye mechi za ligi kuu zinazochezwa Mkwakwani.

Hivyo kutokana na suala hilo tayari uongozi wa Coastal Union umeshamkamata mshabiki mmoja ambaye ni wakala wa kusambaza tisheti hizo kwa mashabiki na kumpeleka polisi na taratibu za kisheria zinaendelea ili kuweza kukomesha vitendo hivyo ambavyo sio vya kiungwana.

Tayari Kampuni ya Pembe Flours Mills ilishasaini mkataba na Klabu ya Coastal Union wa kufadhili kwa kipindi cha mwaka mmoja hivyo Kampuni hiyo kuendelea kufanya matangazo yake kupitia mashabiki hao ni kuvunja utaratibu uliokuwepo.

Hata hivyo tayari Pembe walishatoa jezi 2000 kwa ajili ya kuziuza kwa masabiki mbalimbali wa soka jijini Tanga zilizokuwa na nembo ya pembe na TSN.
Kuhusu suala la Uchaguzi wajumbe wa Kamati hiyo walikubaliana uchaguzi huo ufanyika Novemba 23 mwaka huu ambapo nafasi zitakazojazwa ni Mwenyekiti wa Klabu hiyo na wajumbe wawili wa kamati ya utendaji

Suala la Utiliaji Sahihi wajumbe walilipendekeza fedha zitumike kwenye matumizi yanayofahamika ikiwemo kuwekwa utaratibu wa wazi kwenye matumizi husika.

CHANZO MPENJA BLOG

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC