Ruka hadi kwenye maudhui makuu

ZITTO KABWE KUMALIZA TOFAUTI ZA ALI KIBA, DIAMOND PLUTINUMZ

Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe, amejitosa kusuluhisha ugomvi wa muda mrefu wa wasanii wawili wa muziki wa kizazi kipya nchini, Ali Kiba na Nasibu Abdul 'Diamond'.

Zitto alitoa kauli hiyo juzi wakati akihojiwa katika Kipindi cha Mkasi kinachorushwa na Kituo cha Televisheni cha EATV baada ya kuulizwa kuwa ni jitihada gani amezifanya kusuluhisha ugomvi wa wasanii hao akiwa kama mlezi wa wasanii wanaotoka mkoani Kigoma.


Alisema anafahamu kuwapo kwa ugomvi wa kutoelewana kati ya wasanii Ali Kiba na Diamond na kwamba alishawahi kufanya jitihada za kuwaita kila mmoja kwa nyakati tofauti.

Alifafanua kuwa katika kuhakikisha anawasuluhisha wasanii hao, anaifanya kazi hiyo kwa umakini kwa sababu hataki kuonekana anaingilia maisha ya watu na kwamba ana imani atafanikiwa kuwapatanisha.

Kuhusu madai kwamba ana uhusiano wa kimapenzi na msanii Mwasiti Almas, alisema ni kweli kumekuwapo na uvumi huo lakini kimsingi hana uhusiano wowote wa kimapenzi na msanii huyo.

"Nasikitishwa na madai hayo yanayotolewa na baadhi ya watu, Mwasiti ni kama dada yangu ambaye nimekuwa nikimsaidia katika kazi zake, kuhusishwa naye kimapenzi ni jambo linalonisononesha,"alisema.

Zitto alisema wanaomhusisha katika suala la mapenzi na msanii huyo ni kwa sababu Mwasiti ameimba wimbo ambao amemtaja yeye (Zitto) lakini kiukweli hana uhusiani naye wa kimapenzi.

Alipoulizwa ni lini ataoa, alisema bado 'yupo yupo' na kwamba kuna mwanamke aliyemtaja kwa jina la Jack ambaye amezaa naye mtoto ambaye kwa sasa miaka nane na anasoma darasa la pili nchini Uganda.

 KAMPUNI YA LEKA DUTIGITE

Kuhusu Leka Dutigite inayounganisha wasanii wa Kigoma All Stars, alisema ni kampuni ambayo kila msanii anayetoka mkoani Kigoma ana hisa na ikipata faida wanagawana.

Zitto alisema Leka Dutigite pia inamiliki kampuni nyingine ambayo imekuwa ikipata kazi mfano katika Shirika la Hifadhi za Taifa (Tanapa) na yeye kama mlezi amekuwa akitoa fedha zake kusaidia.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC