Ruka hadi kwenye maudhui makuu

TANZANIA KUANDAA MATAIFA AFRIKA MWAKA 2017

Tanzania imeomba kuandaa Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon) 2017, baada ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF) kuiondoa Libya, iliyokuwa imepangwa kuwa mwenyeji wa michuano hiyo.

CAF ilitangaza kuiondoa Libya kutokana na kukumbwa na machafuko ya kisiasa nchini humo yaliyosababisha kutokuwa na serikali imara.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa (TFF), Selestine Mwesigwa, alisema wametumia nafasi hiyo kuomba kuwa wenyeji wa Afcon 2017.

Mwesigwa alisema uamuzi huo ulifikiwa na kupitishwa na Kamati ya Utendaji ya TFF,  iliyokutana juzi Dar es Salaam kwa lengo la kujadili masuala mbalimbali.

Katibu huyo alisema tayari wamewasiliana na serikali na walitarajia kutuma maombi hayo jana CAF na kwamba wana imani kubwa  ya kukubaliwa,  kutokana na kuwa na sifa za kuandaa fainali hizo.

Alisema miundombinu walionayo inatosha wao kuandaa fainali hizo, hasa ikingizatiwa uwapo wa usalama wa kutosha hapa nchini.Endapo Tanzania itapata nafasi hiyo ya kuandaa michuano ya Afcon, itafuzu moja kwa moja kushiriki kinyang'anyiro hicho kwa sifa ya kuwa timu mwenyeji.

Hiyo itakuwa mara ya pili kwa Tanzania kushiriki michuano hiyo katika historia yake kwani mara mwisho kucheza fainali hizo ilikuwa 1980 wakati huo ikinolewa na Joel Bendera ambaye kwa sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, huku nahodha akiwa ni Rais Mstaafu wa TFF, Leodegar Tenga.

Katika hatua nyingine, Mwesigwa alisema katika kupinga upangaji wa matokeo kwenye mechi mbalimbali za mashindano, endapo akibainika mtu kufanya kitendo hicho atafungiwa maisha kutojihusisha na masuala ya soka.

Kadhalika Mwesigwa alisema Kamati ya Utendaji ya TFF, imemteua Boniface Wambura kuwa Mkurugenzi wa Mashindano  wa shirikisho hilo, kuanzia Septemba Mosi, mwaka huu.

Mwesigwa alisema nafasi aliyokuwa nayo ya Ofisa Habari na Mawasiliano ipo wazi na wametangaza ajira mpya kwa nafasi hiyo.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC