Ruka hadi kwenye maudhui makuu

TAIFA STARS YAKWEPA HUJUMA ZA MAMBAS

Kikosi cha timu ya soka ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars), kinatarajiwa kuwasili leo jioni mjini Maputo tayari kwa mechi yao ya marudiano dhidi ya wenyeji Msumbiji (Mambas) itakayochezwa Jumapili Agosti 3, mwaka huu, huku kikiwa kimejipanga vema kukwepa 'fitna' za ugenini.

Katika kuhakikisha kikosi cha Taifa Stars kinakuwa kwenye mazingira yenye usalama na kuepuka 'hujuma' ya aina yoyote kutoka kwa wenyeji, Shirikisho la Soka nchini (TFF) limetanguliza ujumbe maalumu ili kuweka mipango ya mapokezi vizuri.

Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu, Mwenyekiti wa Kamati ya Ufundi ya TFF, Wilfred Kidao, alisema Stars itawasili jioni Maputo na kila kitu wamekiandaa wao ili kuhakikisha kikosi kinakuwa kwenye mazingira salama.


Mjumbe huyo alisema wanajua mechi hiyo itakuwa na ushindani mkubwa ndiyo sababu wamejipanga kukabiliana na hali hiyo ndani na nje ya uwanja.

"Kila kitu ni cha kwetu, tumeamua kujipanga wenyewe kwa ajili ya timu yetu, hii ni mechi ya kufa au kupona, " alisema kwa kifupi kiongozi huyo bila kueleza kama wameikataa hoteli waliyoandaliwa na wenyeji wao au la.

Alisema pia hali ya hewa ya Maputo kwa sasa inafanana na ya jijini Dar es Salaam wakati kikosi cha Stars kilikuwa kimeweka kambi Tukuyu mkoani Mbeya kwenye baridi na juzi na jana kilikuwa Johannesburg, Afrika Kusini ambapo kwa sasa hali ya hewa ni nyuzi joto 15.

Stars ikiwa Johannesburg, jana ilifanya mazoezi mara mbili (asubuhi na jioni) kwenye Uwanja wa klabu ya Bedfordview Country na leo itafanya mazoezi ya mwisho asubuhi kabla ya kuondoka jioni.

Pia jana jioni wachezaji wa Stars na timu ya vijana umri chini ya miaka 17 (Serengeti Boys) walitarajiwa kukutana na Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Razia Msuya.

Mabao yaliyofungwa na kiungo, Khamis Mcha, yaliifanya Stars kumaliza mechi ya kwanza kwa sare ya mabao 2-2, hivyo inahitaji ushindi wa aina yoyote ili iweze kusonga mbele.

Serengeti Boys iko Johannesburg tangu Jumatatu Julai 27, mwaka huu kwa ajili ya kujiandaa na mechi yao dhidi ya yosso wa nchi hiyo (Amajibos) itakayochezwa kesho Agosti 2, mwaka huu mjini Soweto kuwania nafasi ya kushiriki michuano ya Mataifa ya Afrika chini ya miaka 17 itakayofanyika nchini Niger mwakani wakati Stars yenyewe inasaka tiketi ya fainali za Mataifa ya Afrika zikazofanyika Morocco 2015.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC