Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SIMBA KUSHUKA TENA DIMBANI LEO NA MAFUNZO

Wakati Simba ikitarajia kucheza mechi ya kirafiki leo dhidi ya timu ya Mafunzo ya Zanzibar, kocha Patrick Phiri amesema anatarajia kupata kikosi cha kwanza baada ya Raphael Kiongera kuungana na wachezaji wenzake.

Hii itakuwa ni mechi ya pili ya kirafiki kwa kikosi hicho cha Phiri, baada ya ile ya awali dhidi ya Kilimani City ambayo Simba iliibuka na ushindi wa mabao 2-1.

Akizungumza jana kwa njia ya simu mara baada ya mazoezi ya timu hiyo, Phiri alisema Kiongera anatarajia kuwasili mwishoni mwa wiki, huku kikosi cha kwanza ambacho kitaanza kucheza katika michuano ya Ligi Kuu ya Bara kitajulikana wiki moja kabla ya michuano hiyo kuanza.


Phiri alisema kwa sasa ni vigumu kutangaza kikosi cha kwanza kwa vile wachezaji wengine waliosajiliwa na timu hiyo bado hawajawasili kuungana na wenzao katika mazoezi. Ligi Kuu ya Bara itaanza Septemba 20.

Mzambia huyo alisema kwa sasa pamoja na mazoezi ataendelea kusaka mechi na kirafiki dhidi ya timu zitakazoshiriki Ligi Kuu, kwani zitasaidia kumpa picha ya kile anachopaswa kukitarajia kwenye ligi.

Alisema baada ya mechi ya leo dhidi ya Mafunzo ya Zanzibar itakayopigwa kwenye Uwanja wa Amaan, wanatarajia kucheza dhidi ya Mtibwa Sugar Septemba 6, huku wakiendelea kusubiri mechi ya kirafiki ya kimataifa.

Alisema katika mechi yao ya awali dhidi ya Kilimani City, licha ya kwamba walishinda, hakuridhika na kiwango kilichoonyeshwa na wachezaji wake.

"Bado nahitaji kiwango zaidi katika timu yangu, lengo langu ni kufanya vizuri msimu huu katika ligi kuu ya Bara," alisema Phiri.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...