Ruka hadi kwenye maudhui makuu

RUDISHA AAMBULIA MEDALI YA FEDHA GLASGOW

Rudisha alikuwa bingwa wa Olimpiki mjini London mwaka 2012
Bingwa wa Olimpiki na ambaye pia anashikilia rekodi ya dunia katika mbio za mita 800 mkenya David Rudisha aliambulia medali ya fedhakatika mashindano ya Jumuiya ya madola.


Hii ni baada ya kushindwa na mshindani wake wa karibu Nijel Amos mwenye umri wa miaka 20 katika mashindano hayo yanayoendelea mjini Glasgow Scotland.

Amos, ambaye alishinda medali ya fedha katika mashindano ya olimpiki mjini London alimaliza mbio hizo kwa kishindo baada ya kutoka nyuma ya Rudisha na kumpiku.
Kwa kawaida, Rudisha alikuwa mbele wakati wa mbio hizo kwa mita 150 na kudhibiti mbio zenyewe kama alivyofanya alipovunja rekodi mwaka 2012.

Lakini alikiri kuwa mbio hizo hazikuwa ngumu , ila mita miamoja za mwisho ndizo zilizomtatiza na hapo ndipo Amos aliweza kumpiku Rudisha.
Nigel Amos ana miaka 20
Baada ya kupata jeraha baya la goti mwaka 2013, Rudisha amekuwa mbioni kuuguza jeraha lake na pia umekuwa wakati mgumu wake kwani washindani wake wamekuwa pia wakifanya mazoezi wakilenga kumshinda.

Alionekana kuishiwa na nguvu wakati Amos kutoka Botswana alipompiku na kuanza kusherehekea na kushinda dhahabu.

Rudisha mwenye umri wa miaka 25 alimaliza mbio hizo kwa dakika 1:45.48 nyuma ya Amos huku Andre Olivier wa Afrika Kusini akinyakua Shaba.

Amos aliambia BBC kuwa ana raha sana ingawa Rudisha daima atasalia kuwa bingwa wa mbio za miata 800.
Mbio hizo zilikuwa moja ya mbio zilizosubiriwa kwa hamu kuu katika mashindano hayo ya Jumuiya ya madola.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...