Ruka hadi kwenye maudhui makuu

PHIRI AAHIDI UBINGWA MSIMBAZI, MAXIMO AMTUNISHIA MISULI

Wakati Kocha Mkuu wa Simba, Mzambia Patrick Phiri akidai ubingwa bila kuifunga Yanga hauna raha, Marcio Maximo ametamba kutumia kikosi mseto cha wakongwe na chipukizi kwenye Ligi Kuu Bara iliyopangwa kuanza Septemba 20, mwaka huu.

Akizungumza na gazeti hili kabla ya kuondoka kuelekea visiwani Zanzibar mwishoni mwa wiki ambako Simba imeweka kambi ya kujiandaa na msimu mpya, Phiri alisema moja ya mikakati aliyojiwekea ni kuhakikisha anatwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara lakini hautanoga bila kuifunga Yanga.

"Moja ya mikakati niliyojiwekea ni kuhakikisha Simba inatwaa ubingwa wa ligi ikiwa chini yangu, lakini nitafurahi zaidi nikitwaa ubingwa na kuifunga Yanga," alisema Phiri.


Alisema msimu huu amejipanga kuhakikisha anairejesha raha iliyopotea kwa muda mrefu Msimbazi kwa kuwa mikakati yake ya kwanza ni klabu hiyo kufanya vizuri katika mechi za mzunguko wa wa kwanza na badaye kuhitimisha kwa kutwaa ubingwa.

Phiri ambaye awali katika msimu wa 2004/05 aliipa Simba ubingwa kabla ya ule wa 2009/10 kuhitimisha kwa kutwaa ubingwa bila kupoteza mechi, alisema amejipanga kutoa mazoezi ya makini katika idara zote ili kuwaweka sawa wachezaji wake kabla ya kuanza kwa ligi hiyo.

Mzambia huyo aliondoka jijini Dar es Salaam jana kuelekea Zanzibar kuungana na kikosi cha timu hiyo kwa ajili ya kuendelea na mazoezi ya kujiandaa na Ligi Kuu ya Bara.

Wakati Phiri akieleza hayo, Maximo alisema kikosi chake kipo kamili na mazoezi ya kujiandaa na Ligi Kuu ya Bara na kwamba mazoezi ambayo wameshafanya yamekamilika na kilichobaki ni kurekebisha kasoro ndogo ndogo.

"Timu ipo kamili kwa sasa, imebaki kiasi kidogo kukamilisha mazoezi tayari kwa kuanza Ligi Kuu," alisema Maximo.
Alisema amejipanga kuhakikisha Yanga inafanya vizuri katika michuano hiyo na kutwaa ubingwa ambao kwa sasa unashikiliwa na Azam FC ya jijini Dar es Salaam.

Simba na Yanga zote zimeweka kambi visiwani Zanzibar kwa ajili ya kujiandaa na Ligi Kuu Bara huku mabingwa watetezi Azam FC wakiitumia michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati (Kombe la Kagame) kujiwinda na Ligi Kuu.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC