Ruka hadi kwenye maudhui makuu

NGASSA AWAFUNIKA MBWANA SAMATTA, ULIMWENGU

MSHAMBULIAJI wa Yanga SC ya Dar es Salaam, Mrisho Khalfan Ngassa anaweza akawa mfungaji bora wa Ligi ya Mabingwa Afrika msimu huu, michuano hiyo ikiwa imefikia hatua ya Nusu Fainali.

Taarifa ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF) imesema kwamba, Ngassa hadi sasa anaongoza kwa mabao yake sita baada ya hatua ya awali na ya makundi ya michuano hiyo.Ngassa alicheza mechi nne tu za Raundi mbili za awali za michuano hiyo, dhidi ya Komorozine ya Comoro nyumbani na ugenini, akifunga mabao matatu kila mechi.

Baada ya hapo akacheza vizuri katika mechi zote mbili dhidi ya Al Ahly ya Misri, Yanga SC ikitolewa kwa penalti baada ya sare ya jumla ya 1-1, kila timu ikishinda 1-0 nyumbani kwake.

Lakini tangu hapo, wachezaji waliofanikiwa kumkaribia Ngassa kwa mabao msimu huu kwenye michuano hiyo ni watano, Haithem Jouini wa Esperance ya Tunisia, Edward Takarinda Sadomba wa Al Ahli Benghazi ya Libya, Iajour Mouhssine wa Raja Club Athletic ya Morocco na Knowledge Musona wa Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini, ambao kila mmoja amefunga mabao matano pia, lakini timu zao zimekwishatolewa.Mubele Ndombe wa AS Vita ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), ndiye pekee mwenye mabao matano na timu yake imekwenda Nusu Fainali.


Wenye mabao manne kila mmoja ni Benyoussef Fakhreddine wa Sfaxien ya Tunisia, El Hedi Belameiri wa E. S. Setif ya Algeria, wakati Abdelrahman Ramadan Fetori wa Benghazi ana matatu, sawa na Abdoulaye Ssissoko wa Stade Malien ya Mali, Ahmed Akaichi wa Esperance, Akram Djahnit wa E. S. Setif, Cesair Gandze wa AC Leopards ya Kongo, Driss Mhirsi wa Esperance, Etekiama Agiti Taddy wa AS Vita ya DRC, Kingston Nkhatha wa Kaizer Chiefs na Lamine Diawara wa Stade Malien.
Kwa kuwa michuano hiyo imefikia kwenye hatua ngumu ya Nusu Fainali- ambayo si rahisi timu kufungana mabao mengi,

Ngassa ana nafasi kubwa ya kutawazwa kuwa mfungaji bora msimu huu, licha ya kwamba Yanga SC haikufika hata hatua ya makundi.

 TP Mazembe itakutana na ES Setif ya Algeria katika Nusu Fainali, wakati AS Vita itakutana na CS Sfaxien ya Tunisia, mechi za kwanza zikichezwa kati ya Septemba 19 na 21 na marudiano kati ya Septemba 26 na 28.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC