Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MANGALA SASA NDIYE BEKI GHALI ENGLAND

KLABU ya Manchester City imemfanya Eliaquim Mangala kuwa beki ghali zaidi kwa sasa katika historia ya soka ya Uingereza, baada ya kumnunua kwa Pauni Milioni 31.9 beki huyo wa akti wa Ufaransa kutoka FC Porto.
 
Ndoto za Mangala kuhamia Ligi Kuu ya England hatimaye zilitimia jana baada ya kuupiku uhamisho wa Pauni Milioni 30 uliomtoa Rio Ferdinand Leeds kuhamia Manchester United mwaka 2002.
 
Mangala, mwenye umri wa miaka 23, anakuwa mchezaji wa sita kusajiliwa na City baada ya kukubali Mkataba wa miaka mitano na kocha Manuel Pellegrini anaamini huyo ni moja ya mabeki wa thamani ya juu Ulaya na atadhihirisha thamani yake uwanjani.

MABEKI GHALI LIGI KUU ENGLAND 

Eliaquim Mangala - Pauni Milioni 32- kutoka Porto kwenda Man City, Agosti 2014
Rio Ferdinand - Pauni Milioni 30 kutoka Leeds kwenda Man Utd, Julia 2002
Luke Shaw - Pauni Milioni 27 kutoka Southampton kwenda Man Utd, Juni 2014
Joleon Lescott - Pauni Milioni 22 kutoka Everton kwenda Man City, Agosti 2009
David Luiz - Pauni Milioni 21 kutoka Benfica kwenda Chelsea, Januari 2011
Mfaransa huyo baada ya kukamilisha uhamisho wake amesema; "Mimi ni aina ya mchezaji ambaye naingia uwanjani kushinda,".
"Siachi kitu chochote, wakati wote napambana hadi mwisho na nina matumaini kwa desturi yangu huu, tutashinda mataji mengi msimu huu.
"Nina furaha sasa kwa sababu nitakuwa tayari kuanza maisha mapya. Nitakuwa tayari kufanya mazoezi tena. Ilikuwa vizuri kwenda mapumziko, lakini baada ya muda unarudi kazini.
"Ninakwenda kukimbia kila siku na kufanya mazoezi kwenye gym. Mapumziko ni mazuri, lakini yakiwa marefu, inakuwia vigumu kurudi vizuri. Nafikiri nitahitaji muda, ila nitapambana kurudi katika ubora wangu kwa asilimia 100 haraka iwezekanavyo.
"City ni klabu kubwa Ulaya. Kwangu, ilikuwa hatua muhimu kuondoka Porto na kujiunga na Manchester City ili kusonga mbele kimafanikio. Nataka kushinda mataji na ninaamini nitafanya hivyo,"amesema.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC