Ruka hadi kwenye maudhui makuu

LIVERPOOL NOMA SANA, YAIGONGA SOUTHMPTON 2-1

Kocha wa Liverpool Brendan Rodgers alikuwa na kila sababu ya kutabasamu alipoingia uwanjani Anfield na kuwasikia mashabiki wa klabu hiyo wakishangilia na kuimba nyimbo za kumsifu kwa kuiokoa klabu hiyo msimu uliopita alipoiongoza kumaliza katika nafasi ya pili nyuma ya mabingwa Manchester City.
Lakini wapinzani wao Southampton licha ya kuwa walikuwa wamewapoteza wachezaji watatu kwa mahasimu wao Liverpool hawakuwa wepesi wa kupisha mpira .


Liverpool nayo ilikuwa na kibarua cha kujaza pengo lililowachwa wazi na mfungaji mabao mengi msimu uliyopita katika ligi kuu ya Uingereza Luis Suarez.
mfungaji bao la Liverpool Raheem Sterling
Hata hivyo dakika tisini zilizofuatia ndizo zilizopaswa kuamua mbivu na mbichi.
The reds ndio walioonesha tamaa ya kutaka ushindi na labda kuendeleza msururu wa matokeo mema msimu uliopita.

Juhudi zao zilizaa matunda kunako dakika ya 23 chipukizi Raheem Sterling alipofuma kimiani bao la ufunguzi dhidi ya the saints.
Baada ya nipe nikupe kati ya timu hizo mbili ,mfungaji bao la kwanza Sterling alirejea nyuma katika badiliko la mfumo baada ya kuonekana kuwa safu ya kati ilikuwa imelemazwa na the saints waliokuwa wakiongozwa na Mugabe Wanyama.
Mabadiliko hayo yalimfaa Brendan ambaye alimuingiza Rickie Lambert.
Mfungaji bao la pili la Liverpool D Sturridge
Lambert alichukua pahala pake Philippe Coutinho ambaye alikuwa amekwisha cheza kwa dakika 75 .
Badiliko hilo lilizaa matunda papo hapo Daniel Sturridge alipoifungia Liverpool kunako dakika ya 79 ya kipindi cha pili na kuirejeshea the Reds uongozi wa mechi hiyo.
Mechi hiyo haikuishia hapo kwani Southampton walifanya mashambulizi mara mbili Liverpool ikiokolewa na mwamba wa lango

Mkwaju wa Morgan Schneiderlin uligonga mwamba na kurejea uwanjani kipa wa Liverpool Simon Mignolet akiwa hana jibu lakini juhudi ya kichwa ya Shane Long ikitoka nje na vivyo hivyo matumaini ya the Saints kunusuru japo pointi moja kutoka Anfield.

Hayo yote ni kenda, Liverpool wamesajili ushindi wa mabao mawili kwa moja na kujizolea alama tatu muhimu dhidi ya Southampton katika mechi yao ya kwanza ya ligi kuu msimu huu bila ya mshambulizi wao wa kutegemewa Suarez.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC