Ruka hadi kwenye maudhui makuu

AZAM FC FULL KUIVAA EL MERREIKH KESHO

BEKI Shomary Kapombe na mshambuliaji Lionel Saint- Preux kutoka Haiti wote wamefanya mazoezi kikamilifu jana na leo kuelekea mchezo wa kesho wa Robo Fainali Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame Azam FC ikimenyana na El Marreikh ya Sudan, Uwanja wa Nyamirambo, Kigali, Rwanda.

Wawili hao waliokuwa wanasumbuliwa na maumivu ya nyama za paja, walikosa mchezo wa mwisho wa Kundi A dhidi ya Adama City ya Ethiopia, Azam FC ikishinda 4-1.


Shomary Kapombe katikati (jezi namba nne) akifanya mazoezi kikamilifu na wenzake leo Uwanja wa Kiyovu, Nyamirambo
Azam FC itamenyana na Merreikh kesho Uwanja wa Nyamirambo mjini Kigali.

Na katika mazoezi ya leo asubuhi Uwanja wa Kiyovu, Nyamirambo mjini hapa, kocha Mcameroon Joseph Marious Omog ameonekana kuwahusisha nyota hao katika kikosi kitakachoanza kesho.

Majeruhi mwingine, beki Waziri Salum pia amefanya mazoezi wakati kiungo Himid Mao anatarajiwa kurudi pia baada ya kukosa mchezo dhidi ya Adama kwa sababu ya kadi za njano.
Omog amekuwa akiandaa Azam FC kitaalamu mno kuelekea mchezo huo, akiwaelekeza mifumo na aina tofauti ya uchezaji, ikiwa ni pamoja na kutumia mipira mirefu na mifupi.

Amekuwa akiwandaa pia kwa kupiga penalti, kwa kuwa iwapo mchezo huo utamalizika kwa sare, matuta yataamua timu ya kusonga Nusu Fainali.

Kwa ujumla Azam ambayo imewekwa hoteli moja na wapinzani wao hao, Merreikh, Kigali View eneo la Nyamirambo, ipo vizuri kuelekea mchezo huo, ambao unasubiriwa kwa hamu na Watanzania wengi.

Robo Fainali za Kagame zinaanza leo, mchezo wa kwanza ukiwa kati ya Polisi ya hapa dhidi ya Atleitco ya Burundi, kabla ya Rayon Sport kumenyana na APR, zote za hapa leo, wakati mbali na Azam na Merreikh, mchezo mwingine wa kesho utakuwa kati ya KCC ya Uganda na Atlabara ya Sudan Kusini.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC