Ruka hadi kwenye maudhui makuu

USAJILI ULAYA WAZIDI KUPAMBA MOTO

Manchester United wamerejea tena kumfuatilia winga wa Real Madrid Angel Di Maria, 26, baada ya jaribio la kwenda Paris Saint Germain kugonga mwamba kuhusiana na ada ya uhamisho ya pauni milioni 45 (Sun)

Southampton wanataka kubaki na kiungo wao Morgan Schneiderlin, 24, na watawaambia Tottenham na Arsenal watahitaji kutoa zaidi ya pauni milioni 27 kama wanamtaka (Guardian)

Boss mpya wa Southampton, Ronald Koeman amekataa pauni milioni 3.25 kutoka Cardiff kumsajili beki Jose Fonte, 30 (Daily Mirror)


Barcelona wanafikiria kumchukua beki wa kati Thomas Vermaelen, 28, kutoka Arsenal, ambaye pia anasakwa na Manchester United (Sun), Arsenal wamepewa nafasi ya kumsajili mshambuliaji wa AC Milan Mario Balotelli, 23, kwa pauni milioni 7.9 pamoja na kubadilishana na winga kutoka Costa Rica, Joel Campbell (Metro)

QPR wanazungumza na Marseille kumchukua kiungo wa Ufaransa Mathieu Valbuena, 29, ingawa Dynamo Moscow pia wanamtaka (Daily Mirror), Everton wana matumaini ya kukamilisha uhamisho wa pauni milioni 18 wa mshambuliaji wa Chelsea, Romelu Lukaku, 21 baada ya kuwasili kwa Didier Drogba, 36, Darajani (Daily Express)

Everton pia wanatazama uwezekano wa kumsajili mshambuliaji wa Monaco Lacina Traore, 23, kwa mkopo (Times), boss wa Roma Rudi Garcia amesema kiungo Kevin Strootman, 24, hana mpango wa kwenda Mancheter United msimu huu (Sky Sports)

Liverpool wametoa dau la pauni milioni 14.2 kumtaka winga wa Bayern Munich Xherdan Shaqiri, 22 (Daily Star), West Ham wamekuwa na mazungumzo na mshambuliaji wa Besitkas Hugo Almeida, 30, baada ya Andy Carroll kuumia (Times)

Atlètico Madrid wanamtaka mshambuliaji wa Real Sociedad, Antoinne Griezmann, ambaye anafuatiliwa na Tottenham pia (Daily Express), mshambuliaji wa Manchester United Wayne Rooney, 28, anataka kuwa nahodha wa klabu hiyo na anaamini huenda akalibeba Kombe msimu unaokuja (Manchester Evening Standard)

Kiungo wa Man U Tom Cleverly, 24, ana uhakika atarejea katika 'form' chini ya Louis van Gaal baada ya kuwa na wakati mgumu enzi za David Moyes (ESPN), Wojciech Szcesny, 24, atasalia kuwa kipa namba moja wa Arsenal licha wa kuwasili kwa David Ospina, 25 kutoka Nice (Daily Express)

Chelsea bado wanamfuatilia beki wa Real Madrid Rafael Varane, ambaye yupo katika mazungumzo juu ya mkataba mpya (The Independent), Real Madrid huenda wakamchukua mshambuliaji wa Colombia Radamel Falcao kwa mkopo na mshahara wa euro milioni 12 kwa mwaka (ABC)

Everton wanamfuatilia kwa makini winga wa AIK Nabil Bahoui, 23 (Sky Sports), Edinson Cavani anataka kuondoka Paris Saint-Germain, huku Manchester United wakiwa wanamtazama mchezaji huyo wa Uruguay (Le 10 Sport)

Hatma ya Angel Di Maria inatarajiwa kuamuliwa siku chache zijazo, huku Real Madrid wakiwa tayari kupokea dau la euro milioni 50 hadi 60 kutoka kokote (Cadena Cope)

Liverpool huenda wakamkosa Divock Origi baada ya Atlètico Madrid kumtaka mchezaji huyo wa Ubelgiji, kufuatia kuondoka kwa Diego Costa, Adrian na David Villa (Marca) Arsenal wanakaribia kumsajili beki Calum Chambers kutoka Southampton (Sky Sports)

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC