Ruka hadi kwenye maudhui makuu

STRAIKA WA IVORY COAST AMALIZANA NA SIMBA

Mshambuliaji wa timu ya soka ya Taifa ya Burundi, Pierre Kwizera, ambaye alikuwa nchini akifanya mazungumzo na uongozi wa Simba, ameondoka juzi usiku kurejea Ivory Coast kwa lengo moja la kwenda kuvunja mkataba na klabu yake ya Afad Abdijan.

Mchezaji huyo anayecheza nafasi zaidi ya mbili uwanjani, amewaambia viongozi wa Simba kwamba atahakikisha anamalizana na Afad Abdijan na kurejea jijini Dar es Salaam kuitumikia klabu hiyo katika msimu ujao wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara.

"Kuna mambo naenda kumalizia huko, ila nitarudi Tanzania kucheza Simba," alisema kwa kifupi mchezaji huyo.

Habari kutoka uongozi wa Simba zinaeleza kuwa mchezaji huyo atarejea jijini Agosti 28, mwaka huu tayari kuanza mazoezi na wachezaji wenzake wa timu hiyo.


Kiongozi huyo alisema kuwa Kwizera, amepanga kumalizana kwa busara na viongozi wake wa klabu hiyo ya Ivory Coast ndipo asaini mkataba mpya na Simba.

"Ila ametuhakikishia anarejea Simba," alisema kiongozi huyo ambaye ni Mjumbe wa Kamati ya Utendaji na Kamati ya Usajili.
Simba inajipanga kuimarisha kikosi ili iweze kurejesha heshima yake iliyopoteza msimu uliopita kwa kumaliza ikiwa katika nafasi ya nne kwenye msimamo wa ligi.

Pia, Simba bado iko katika mipango ya kumnasa kiungo mshambuliaji wa timu ya KCB na timu ya Taifa ya Kenya (Harambee Stars), Paul Kiongera.

Rais wa Simba, Evans Aveva, yupo Nairobi, Kenya kukamilisha mazungumzo na nyota huyo ambaye alishawahi kufanya kazi na Kocha Mkuu wa Simba, Zdravko Logarusic, katika timu ya Gor Mahia.

Azam ndio mabingwa wa msimu uliopita huku Yanga ikiwa ya pili na timu iliyoshiriki kwa mara ya kwanza, Mbeya City, ilimaliza ligi ikiwa ya tatu.

Kikosi cha Simba cha msimu ujao kitatambulishwa rasmi katika Tamasha la Simba Day ambalo mwaka huu litafanyika Agosti 9 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC