Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SIRI YA KUTEMWA BIN KLEB YANGA HII HAPA....

WAKATI kukiwa kuna sintofahamu juu ya Mwenyekiti wa klabu ya Yanga SC, Yussuf Manji kuunda Kamati mpya ya Utendaji ya klabu hiyo akiwaweka nje Wajumbe kadhaa, akiwemo Abdallah Bin Kleb, imefahamika kiongozi huyo aliomba mwenyewe kujitoa.

Ingawa sababu haswa ya Bin Kleb kujitoa haijulikani, lakini chanzo cha karibu na aliyekuwa Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Yanga na Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano, kimesema kwamba sababu za kupata muda wa kutosha kwa ajili ya biashara zake.

“Abdallah kwa muda mrefu alikuwa anaomba udhuru ili kushughulikia biashara zake ambazo zilikuwa zinakosa usimamizi wa uhakika kutokana na muda wake mwingi kufanya kazi za Yanga,”.


“Shughuli za Dar es Salaam alikuwa anazisimamia vizuri, lakini zile za nchi jirani zilikuwa zinakosa usimamizi kwa sababu muda mwingi yupo na Yanga, kabla ya mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu (msimu uliopita) aliomba udhuru,”.

“Na baada ya mzunguko wa kwanza pia aliomba udhuru, yote kwa sababu ya kwenda kusimamia biashara zake, sasa baada ya kuona kabisa bila kujitoa moja kwa moja, biashara zake zitayumba akamuomba Manji mapema, akiteua Kamati mpya, yeye asimuweke,”kimesema chanzo hicho.

“Manji alimkatalia mara ya kwanza, lakini ikafika wakati ikabidi amkubalie kwa sababu yeye mwenyewe Abdallah ameahidi kuendelea kuusaidia uongozi kila atakapokuwa anapata nafasi,”kimeongeza chanzo hicho.

Bin Kleb aliingia kwa pamoja na Manji, Makamu Clement Sanga na Wajumbe George Manyama na Aaron Nyanda katika uchaguzi mdogo mwaka juzi, akiwa mgombea aliyepata kura nyingi zaidi ya wengine wote.

Na katika kipindi chake, aliiwezesha Yanga kusajili wachezaji wa kiwango cha juu kama Haruna Niyonzima, Mbuyu Twite, Kevin Yondan, Frank Domayo, Didier Kavumbangu, Emmanuel Okwi, Juma Kaseja na wengineo.

Akiwa Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano pia, chini yake Yanga SC ilitwaa ubingwa wa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame na Ligi Kuu pamoja na kuweka rekodi ya kuifunga kwa mara ya kwanza timu ya Misri, kwenye michuano ya Afrika, Al Ahly 1-0 mwaka huu.
 
Bin Kleb akiwa ameshika kwa pamoja Kombe la Kagame na Sanga
Seif Magari kushoto akimpongeza Bin Kleb kwa kufanikisha kumrejesha Mrisho Ngassa Yanga. Kulia kabisa ni Mussa Katabaro
Wanachama wengi wa Yanga SC bado wanaamini Bin Kleb kwa kushirikiana na ‘sahiba’ wake Ahmed Seif ‘Magari’ ndio wanaweza kupambana na Friends Of Simba ambao kwa sasa wameshika hatamu Simba SC.

Wana Yanga pia bado wanaamini kukosekana kwa Bin Kleb itakuwa pigo kwenye klabu hiyo, hususan katika sekta ya ‘fitna’ dhidi ya wapinzani wao kwenye utawala wa soka ya Tanzania kwa ujumla, Simba SC.
 
Jana, Mwenyekiti wa Yanga SC, Yussuf Manji alitangaza Kamati mpya ya Utendaji ya klabu hiyo, ambayo pamoja naye kama Mwenyekiti na Sanga Makamu wake, Wajumbe ni Abubakar Rajabu atakayesimamia pia Mradi wa Jangwani City, Sam Mapande atakayesimamia pia Sheria na Utawala Bora, George Fumbuka atakayesimamia pia Uundwaji wa Shirika, Waziri Barnabas atakayesimamia pia Vibali vya Hatimiliki na Mahusiano na Wafadhili, Abbas Tarimba atakayesimamia pia Mipango na Uratibu, Isaac Chanji na Seif Ahmed ‘Magari’ watakaosimamia pia Uendelezaji wa Mchezo, Mussa Katabalo atakayesimamia pia Mauzo ya Bidhaa, Mohammed Bhinda atakayesimamia pia Ustawishaji wa Matawi, David Ndeketela Sekione atakayesimamia pia Uongezaji wa Wanachama, Mohammed Nyenge atakayesimamia pia Utangazaji wa Habari, Taarifa na Matangazo.

Wajumbe hao, pia wataongoza Kamati ndogo ndogo, Mapande za Kamati ya Maadili, Nidhamu na Uchaguzi, Fumbuka na Barnabas Kamati ya Uchumi na Fedha Chanji na Magari Kamati za Ufundi, Mashindano naSoka la Vijana na Wanawake.

Wajumbe waliotemwa mbali na Bin Kleb ni Salum Rupia, Manyama, Nyanda na Lameck Nyambaya.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC