Ruka hadi kwenye maudhui makuu

NIGERIA KUTETA NA STEPHEN KESHI

Shirikisho la kandanda la Nigeria NFF limesema kuwa linaanda mikakati ya kufanya mazungumzo na aliyekuwa kocha wa timu ya taifa Super Eagles Stephen Keshi wakimtaka aendelee kuhudumu kama mkufunzi mkuu. 


Kauli hii mpya ni tofauti na ile iliyochukuliwa na afisi iliyokuwepo awali ambayo ilikataa kuandikisha kandarasi upya naye.

Hata hivyo waziri wa michezo wa Nigeria anasemekana hakufurahishwa na matakwa mapya ya nyongeza ya mshahara alioitisha Keshi.

Keshi anasemekana kuwa aliomba kuongezewa mshahara wake maradufu hadi kutimia dola elfu thelathini ($30,000) kwa mwezi na kuwa pesa hizo zilipwe kabla hajaanza hatamu mpya.
Uongozi wake kocha Keshi umekumbwa na migomo ya mara kwa mara kuhusiana na malimbikizi ya marupurupu ya wachezaji na mishaharaa yao.

Keshi hata hivyo anakumbukwa kwa kuingoza The Super Eagles kunyanyua kombe la mabingwa barani Afrika mwaka wa 2013 mbali na kutimu raundi ya pili ya kombe la dunia la mwaka huu lililokamilika huko Brazil mapema mwezi huu.
Maigari Aminu amen'golewa madarakani Nigeria
Kamati kuu ya NFF hata hivyo imeagiza mazungumzo yaanze kwa niya ya kuandikisha upya kandarasi naye katika kipindi cha juma moja lijalo.

Wakati huohuo waziri wa michezo Tammy Danagogo amewaasa wadau wa kandanda nchini humo kuzika tofauti zao na kuimarisha viwango vya kandanda .

Danagogo alisema kuwa maafisa hawana budi kusitisha malumbano na vita vya kungangania uongozi kwa niya ya kujifaidisha .

Waziri aliyasema hayo muda mchache baada ya kamati kuu ya NFF kumn'goa mamlakani mwenyekiti wa shirikisho hilo

Aminu Maigari kwa madai ya ufujaji fedha za shirikisho.
Kamati hiyo ilichukua hatua hiyo takriban juma moja baada ya mapatano kati yao na shirikisho la soka duniani FIFA kumrejesha mamlakani baada ya mahakama moja kumng'oa uongozini.

Makamu wake , Chief Mike Okeke Umeh, ndiye atakayechukua hatamu kama kaimu mwenyekiti wa NFF hadi uchaguzi ujao utakaofanyika Agosti tarehe 26.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...