Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MBWANA SAMATTA ATUMA SALAMU ZA POLE KWA BRAZIL

Straika wa kimataifa Mbwana Samata wa Tanzania, amesema atatua nchini Julai 16 (Jumatano ijayo) ili kuongeza nguvu katika kikosi cha Taifa Stars kinachojiandaa kuikabili Msumbiji kuwani tiketi ya kushiriki fainali zijazo za Mataifa ya Afrika (AFCON).

Samata ambaye alikuwa na majeraha yaliyomfanya akose mechi ya marudiano ya Taifa Stars dhidi ya Zimbabwe mwezi uliopita, amesema kwa sasa yupo fiti japo hajacheza mechi yoyote tangu apone.

“Nitakuja kambini tarehe 16, inshallah panapo majaliwa, ninaendelea vizuri kwa sasa japokuwa sijacheza mchezo wowote tangu nilipotoka katika maumivu,” alikaririwa Samata jana na moja ya mitandao ya michezo nchini.


Samata, mshambuliaji wa mabingwa mara nne wa Afrika, Klabu ya TP Mazembe ya DR Congo, ni mmoja kati ya wachezaji muhimu wa Taifa Stars katika kipindi cha miaka mitatu sasa na atatua nchini kuungana na kikosi hicho cha kocha Martin Nooij kilichoweka kambi mjini Tukuyu, Mbeya.

Stars itacheza dhidi ya Msumbiji Jumapili Julai 20, mwaka huu katika mechi ya kwanza ya hatua ya pili ya mtoano ili kuingia katika hatua ya makundi ya fainali hizo zitakazofanyika Morocco mwakani.

KIPIGO BRAZIL

Aidha, Samata amesema kipigo cha mabao 7-1 ambacho timu ya taifa ya Brazil imekipata kutoka kwa Ujerumani ni aibu lakini matokeo hayo yachukuliwe kuwa sehemu ya mpira wa miguu.

Ujerumani iliwapiga bila huruma wenyeji hao wa Fainali za Kombe la Dunia mwaka huu katika mechi ya nusu fainali usiku wa kuamikia juzi.
"Hakika Brazil wamepata aibu kubwa ukizingatia ni wenyeji, ila ndiyo mpira ulivyo," alisema Samata.

Wakati huo huo, viungo Jonas Mkude (Simba) na Himid Mao (Azam) wameanza mazoezi na Taifa Stars huko Tukuyu, Mbeya baada ya kupona majeraha yaliyokuwa yakiwasumbua.

Daktari wa timu hiyo, Billy Haonga jana alilithibitishia NIPASHE  kupona kwa wachezaji hao na kuanza kufanya mazoezi, Mkude alikuwa akisumbuliwa na majeraha ya goti wakati Mao alikuwa na maumivu ya nyama za paja.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC