Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MAXIMO AMREJESHA NSAJIGWA YANGA

KOCHA mpya wa Yanga SC, Mbrazil Marcio Maximo amemrejesha beki wa zamani wa timu hiyo, Nsajigwa Joel Shadrack Mwandemele ‘Fusso’ katika timu hiyo.

Maximo alifanya kazi na Nsajigwa katika miaka yake minne ya kuifundisha timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars na alimpa Unahodha katika miaka yake miwili ya mwisho.

Hiyo ilifuatia kustaafu kwa Manahodha wake wawili wa awali, kwanza Mecky Mexime na baadaye Salum Swedi ‘Kussi’ na Nsajigwa aliendelea kuwa Nahodha wa Stars mbele ya kocha aliyemfuatia Maximo, Jan poulsen kabla ya kustaafu mwaka jana.


Na baada ya kurudi Tanzania kama kocha wa Yanga SC, Maximo amemkumbuka askari wake huyo wa zamani na kumrejesha Jangwani, ingawa safari hii harejei kama mchezaji, bali kocha.

Maximo amemrejesha Nsajigwa Yanga ili awe kocha wa kikosi cha vijana wa timu hiyo, maarufu kama Yanga B, wakati aliyekuwa kocha wa timu hiyo, Salvatory Edward Augustino ‘Doctor’ anaingia kwenye benchi la ufundi la kikosi cha kwanza.

Maximo amevutiwa na utendaji wa kiungo wa zamani wa Yanga SC, Salva na ameona bora awe naye moja kwa moja kama Msaidizi wake wa kikosi cha kwanza na timu ya pili, iende kwa Nsajigwa.

Juma Pondamali ‘Mensah’ anaendelea kuwa kocha wa makipa, wakati Mbrazil mwingine, Leonardo Neiva anaendelea kuwa kocha Msaidizi Mkuu.

Yanga SC kwa sasa ipo kweye mazoezi makali, ikijiandaa na michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame, inayotarajiwa kuanza mapema mwezi ujao mjini Kigali, Rwanda.

Yanga SC inatarajiwa kuingia kambini Bagamoyo wakati wowote kwa maandalizi zaidi ya michuano hiyo, ambayo wamepangwa kundi A pamoja na wenyeji, Rayon Sport, KMKM ya Zanzibar, Coffee ya Ethiopia na Atlabara ya Sudan Kusini.

Kundi B lina timu za APR ya Rwanda, KCC ya Uganda, Flambeau de L’Est ya Burundi, Gor Mahia ya Kenya na Telecom ya Djibouti, wakati Kundi C linaongozwa na mabingwa watetezi, Vital’O ya Burundi, El Merreikh ya Sudan, Polisi ya Rwanda na Benadir ya Somalia.

Timu 14 zinatarajiwa kushiriki michuano hiyo kuanzia Agosti 8 hadi 24 mwaka huu- jumla ya mechi 34 zikichezwa katika viwanja vya Amahoro na Nyamirambo, Kigali.

Nsajigwa alikuwa Nahodha wa Stars wakati wa Maximo, hapa anakabiliana na Robinho katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Brazil

Rais Paul Kagame wa Rwanda ndiye mlezi wa mashindano haya ambaye hutoa dola za Kimarekani 60,000 kila mwaka kwa ajili ya zawadi.

Wizara ya Michezo ya Rwanda na mashirika mengine yatadhamini michuano hiyo, itakayokwenda sambamba na maazimisho ya miaka 20 ya mauwaji ya kimbau.

Televisheni ya kulipia ya Supersport ya Afrika Kusini ambao ni maswahiba wa muda mrefu wa CECAFA, ni miongoni mwa wadhamini pia na wataonyesha mechi zote za michuano hiyo moja kwa moja. Ratiba ya mashindano hayo inatarajiwa kutolewa wiki hii.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC