Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MALINZI AWASUTA MAREFA WA TANZANIA, ADAI WAMESHAMIRI RUSHWA

RAIS wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amesema kwamba sekta ya marefa nchini inatia aibu kwa sababu ipo chini mno na amewataka viongozi wa sekta hiyo kuhakikisha wanaiinua juu.

Akizungumza wakati wa kufunga semina ya marefa wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Malinzi amesema kwamba ipo haja ya jitihada kubwa kufanyika kuinua sekta hiyo.


Malinzi amesema baadhi ya nchi jirani ikiwemo Kenya zilikuwa na marefa katika Kombe la Dunia mwaka huu nchini Brazil, lakini Tanzania haikuwa na refa hata mmoja.Amesema hata kwenye michuano mingine ya barani, kama Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) bado ushiriki wa marefa wa Tanzania ni duni.

Malinzi ameshauri vyuo vya elimu ya juu nchini navyo visaidie kutoa mafunzo ya urefa, akitolea mfano Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) ambao wana somo la Elimu ya Viungo inayohusu mwili wa mwanamichezo (PE).

“Mfano pale UD (Chuo Kikuu Dar es Salaam) wana somo la PE, kama wataamua kutoa mafunzo ya urefa sisi (TFF) tutakuwa tayari kuwapa ushirikiano ili kuhakikisha tunainua viwango vya marefa nchini,”amesema Malinzi.

Malinzi amesema kwamba amesikitishwa na mkoa wa Ruvuma alipoutembela hivi karibuni na kukuta una marefa wanane tu, wakati ni mkubwa na una wilaya nyingi.
 “Nilishangaa sana, mkoa mkubwa kama ule una marefa wanane tu, sasa huyo bingwa wa mkoa anapatikana vipi, kwa kweli hali ni mbaya sana,”amesema.

Malinzi amesema baada ya hali hiyo, ameagiza TFF ifanye tathmini ya kujua kila mkoa una marefa wangapi ili kujua sehemu ambazo wana mapungufu waelekeze nguvu ya kuinua marefa.

Amesema ipo haja ya waamuzi wastaafu, wakongwe na viongozi wa marefa kushirikiana kuinua marefa chipukizi katika viwango vizuri ili taifa liwe na marefa wa kutosha siku za usoni.

Pamoja na hayo, Malinzi amewaasa marefa kujiepusha na rushwa- kwani soka ya Tanzania kwa sasa inanyemelewa na maharamia wa kimataifa wa kupanga matokeo ili kujinufaisha katika mchezo wa kamari.

“Nina ushahidi wa kutosha mechi za Tanzania sasa zinachezewa kamari nje ya nchi, sasa hii ni hatari sana kwa soka yetu, naomba sana mjiepushe na upangaji wa matokeo,”amesema.

Malinzi amesema TFF inawafanyia uchunguzi marefa wawili kwa tuhuma za kupanga matokeo ambao kwa sasa wamesimamishwa ili kupisha uchunguzi huo, na ikibainika ni kweli watachukuliwa hatua kali za kisheria.

“Nchi za wenzetu ukigundulika ulihusika na upangaji wa matokeo, unapelekwa mahakamani sheria inafuata mkondo wake, sasa na sisi tutafanya nini, kwa hiyo naomba sana tujiepushe na upangaji wa matokeo,”Malinzi aliwaambia marefa huyo.

Semina hiyo iliendeshwa na mkufunzi wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA), Carlos Henriuques kutoka Afrika Kusini ambaye ni Ofisa Maendeleo ya Marefa wa shirikisho hilo.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...