Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MAKALA: HUSSEIN SHARRIF CASSILAS KUSAJILIWA KWAKE SIMBA NA NDOTO YA KUWA TANZANIA ONE

Na Prince Hoza

JANA Simba SC ilifanya usajili wa wachezaji watatu kwa mkupuo, wamo walinda milango wawili ambao ni Hussein Sharrif 'Cassilas' na Peter Manyika mtoto wa kipa wa zamani wa Yanga na timu ya taifa Manyika Peter Manyika.

Usajili huo ulienda sambamba na mchezaji mwingine aitwaye Hajibu, lakini usajili wa Cassilas ndio ulioweza kushtua zaidi hasa kutokana na ubora wake awapo uwanjani.


Cassilas ndiye kipa bora wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara msimu wa 2013/14 akiwashinda walinda milango wote nchini, ligi ya bara imekuwa na changamoto zake katika suala la ushindani lakini Cassilas ameweza kuvuka.

Ligi kuu ya bara ilishirikisha makipa bora na mahiri lakini wote hawakuweza kufua dafu kwa Cassilas ambaye alikuwa anaiongoza Mtibwa Sugar ya Turiani Morogoro inayotumia uwanja wake wa Manungu.

Kati ya makipa walioshiriki ligi kuu bara ni pamoja na Juma Kaseja, Aishi Manula, Shaaban Kado, Ally Mustapha 'Barthez', Deogratus Munishi 'Dida', Ivo Mapunda na wengineo.

Cassilas anastahili pongezi kwa kufanikiwa kutajwa kipa bora nchini, uongozi wa klabu ya Simba chini yake Evans Elieza Aveva umeanza kazi kwa kishindo, kwanza ilianza kutembelea uwanja wa klabu hiyo uliopo Bunju, pili umeanza kufanya usajili.

Simba imekuwa na tatizo kubwa hasa katika sehemu ya mlinda mlango, mpaka ligi kuu ya bara inamalizika kilio kikubwa cha mwalimu wa timu hiyo Zdravko Logarusic ni mlinda mlango na beki wa kushoto.

Loga amekuwa akilalamika kuwa Simba inahitaji mlinda mlango mwingine wa kuweza kumletea ushindani kipa aliyepo Ivo Mapunda, Ivo Mapunda amekuwa akicheza peke yake kufuatia kutoridhishwa kwa udakaji wa Yaw Berko na chipukizi Abou Hashimu.

Hivyo Loga akapendekeza asajiliwe kipa mwingine, mawazo yalielekezwa kwa makipa wawili wa ndani ambao ni Ally Mustapha Barthez au Hussein Sharrif 'Cassilas'.

Hata hivyo mipango ya kumchukua Barthez ilishindikana kufuatia uongozi wa Yanga kumpa tena mkataba kipa wake Ally Mustapha 'barthez', awali Barthez alitangazwa kutemwa kutokana na kuifungisha Yanga ilipocheza na Simba katika mchezo wa ligi kuu Tanzania bara mzunguko wa kwanza Oktoba 20 uliochezwa uwanja wa Taifa ambapo Yanga na Simba zilitoka sare ya kufungana 3-3.

Matokeo hayo yaliwakera Wana-Yanga ambapo ikamlazimu Barthez kuchunguzwa na kutuhumiwa kuihujumu timu yake, Barthez alikuwa akipigiwa hesabu kurejea Simba lakini mipango hiyo ikashindikana.

Ndipo kamati ya usajili ya Simba ikiongozwa na Zakaria Hanspoppe na makamu wake Kassim Dewji 'Mzee wa fitina' walipoanza kuwania saini ya Cassilas.

Dili ilikamilika Alhamis ambapo mjumbe wa kamati ya usajili ya klabu hiyo Said Tully alipoweza kukamilisha kazi ya kumleta kipa bora wa ligi kuu bara Hussein Sharrif maarufu kama Cassilas.

Cassilas akiwa na mjumbe wa kamati ya usajili Said Tully baada ya kumwaga wino Simba.

Ujio wa Cassilas ndani ya Simba unaweza kutimiza ndoto za Loga kuwa na makipa wawili wenye uwezo unaofanana au kuzidiana, pia kuongezeka kwa kipa mwingine ambaye pia ni bora Peter Manyika kunaifanya Simba kukamilisha usajili wake wa makipa.

Hata hivyo mlinda lango Hussein Sharrif 'Cassilas' amefurahia ujio wake ndani ya Simba huku akisema ni furaha kwake, kujiunga Simba ni furaha katika maisha yake kwani aliwaza siku moja kuichezea timu hiyo.

Imekuwa ni bahati sana kwa mchezaji wa mpira wa miguu kupata nafasi ya kuchezea moja kati ya vilabu vikubwa na vikongwe nchini, hakutegemea kama atasajiliwa na Simba kwani licha ya kuipenda timu hiyo lakini ukubwa wa timu hiyo utamfikisha mbali.

Akizungumzia ndoto zake za kuwa Tanzania One, anasema sehemu pekee itakayomfanya kuzitimiza ndoto hizo ni Simba peke yake, ana imani kubwa atakuwa katika kikosi cha kwanza lakini amesema atapata ushindani mkubwa kutoka kwa makipa wenzake.

Amedai hatowaangusha mashabiki wa timu hiyo pindi tu akipata nafasi ya kucheza kwani anajua Simba ni timu kubwa na yenye mashabiki wengi kuliko aliyopata kuichezea ya

Mtibwa Sugar, pia ndoto zake za kucheza soka la kulipwa ughaibuni inaweza kutimia akiwa Simba.Umaarufu wa klabu hiyo nje ya mipaka ya Tanzania kunaweza kumfanya asajiliwe haraka, Mtibwa Sugar haijulikani nje ya nchi na ndio maana hakupata kusajiliwa nchini DRC-Congo licha ya kufuzu majaribio.

Lakini ukubwa wa timu ya Simba na ushawishi wake unaweza kumfanya apate maisha mapya ya soka na kufurahia kipaji chake, Cassilas anatajwa kama kipa bora kuliko hata Dida lakini alishindwa kuchaguliwa timu ya taifa kutokana na kutokuwa katika klabu kubwa nchini.
Ni suala la kusubiri kisha tuone, 0652 626627.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC